Figo zenye uzito wa kilo 35 zatolewa katika upasuaji

Muhtasari

• Warren mwenye umri wa miaka 54 kutoka eneo la Windsor ,Berkshire anaugua ugonjwa kwa jina Polycystic kidney .

Mtu anayeaminika kuwa na figo kubwa zaidi duniani amezungumza kuhusu juhudi zake za kuendelea na maisha yake kufuatia upasuaji wa kuziondoa.

Warren mwenye umri wa miaka 54 kutoka eneo la Windsor ,Berkshire anaugua ugonjwa kwa jina Polycystic kidney .

Ugonjwa huo unaorithiwa husababisha uvimbe kukua katika figo hali ambayo inawezi kuzifanya figo hizo kushindwa kutekeleza majukumu yake.

Ugonjwa huo huathiri mtu mmoja kati ya 1000 na hauna tiba. BBC ilikutana na Warren wiki chache zilizopita kabla ya kufanyiwa upasuaji katika hospitali ya Churchill mjini Oxford na ikakutana naye tena baada ya miezi mitatu.