Siku ya Ukimwi Duniani: ‘unyanyapaa na ubaguzi bado upo’

Maafisa wa afya walifahamu kwa mara ya kwanza kuhusu Ukimwi katika majira ya kiangazi mwaka wa 1981.

Muhtasari

• Dawa za kupunguza makali ya virusi sasa yanapatikana kila mahali lakini mafanikio sio sawa.

• Umoja wa Mataifa unasema, huku 76% ya watu wazima kwa ujumla walipokea dawa hizo -antiretrovirals  katika mwaka  2021, ni  52% pekee ya watoto (wa miaka kuanzia 0-14 ) waliopata tiba hiyo.

Martha yuko wazi sana kuhusu hali yake ya HIV. Kuwa muwazi kwake kumemsaidia kupata usaidizi zaidi wa kihisia
Martha yuko wazi sana kuhusu hali yake ya HIV. Kuwa muwazi kwake kumemsaidia kupata usaidizi zaidi wa kihisia
Image: MARTHA CLARA NAKATO

Maafisa wa afya walifahamu kwa mara ya kwanza kuhusu  Ukimwi katika majira ya kiangazi mwaka wa  1981.

Katika miaka ya 1980, Kwa mtu kupatikana na Ukwimwi ilionekana kama  'waranti ya kifo' lakini kutokana na  maendeleo na sayansi ya matibabu, inawezekana sasa kwa kiasi kikubwa kwa wagonjwa wanaoishi na virusi vya HIV kuishi maisha ya afya.

 Lakini Umoja wa Mataifa unasema kwamba watoto wanaoishi na virusi vya HIV hawapati msaada unaofaa. Tulizungumza na vijana watatu wanaoishi na HIV.

"Dunia inaendelea kushindwa kuwasaidia watoto katika kukabiliana na Ukimwi. Maambukizi mapya miongoni mwa watoto yanaweza kuzuiwa lakini  bado watoto 160,000  walipata maambukizi mapya mwaka  2021," anasema Fodé Simaga,  Mkurugenzi wa , Global Practice Science, Systems na  Services for All, UNAIDS.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa , zaidi ya watu milioni wameambukizwa tangu mwanzoni mwa janga na zaidi ya watu milioni 40 walikufa kutokana na magonjwa yanayohusiana na Ukimwi.

Ikilinganishwa na siku za mwanzo wa janga, dawa za kupunguza makali ya virusi sasa zinapatikana kila mahali lakini mafanikio sio sawa.

Umoja wa Mataifa unasema, huku 76% ya watu wazima kwa ujumla walipokea madawa hayo -antiretrovirals  katika mwaka  2021, ni  52% pekee ya watoto (wa miaka kuanzia 0-14 ) waliopata tiba hiyo.

BBC ilizungumza na vijana watatu kutoka nchi tofauti , wanaoishi na virusi vya HIV. 

'Mtoto wangu hatazaliwa na HIV'

Martha Clara Nakato ni msichana Mganda mwenye umri wa miaka 26 anayeishi mjini Kampala. Alipatikana na Ukimwi alipokuwa na umri wa miaka 14 pekee.

Mnamo mwaka 2019, Martha alikuwa mmoja kati ya watu watano waliochukuliwa kama kielelezo cha mpango wa kielelezo cha dunia cha mapambano ya Ukimwi “ Global faces of the Fight” kwa ajili ya kujaza tena hazina ya dunia – ulioanzisha kampeni ya kuchangisha pesa za vita dhidi ya Ukimwi uliochangisha dola bilioni 14.
Mnamo mwaka 2019, Martha alikuwa mmoja kati ya watu watano waliochukuliwa kama kielelezo cha mpango wa kielelezo cha dunia cha mapambano ya Ukimwi “ Global faces of the Fight” kwa ajili ya kujaza tena hazina ya dunia – ulioanzisha kampeni ya kuchangisha pesa za vita dhidi ya Ukimwi uliochangisha dola bilioni 14.
Image: MARTHA CLARA NAKATO

Kaka yake ambaye ni pacha wake alishiriki ngono bila kinga na alikuwa na wasiwasi. Walikwenda kwenye kituo cha kupima HIV wakiwa pamoja. Kwasababu  kupima ugonjwa ilikuwa ni bure, pia alipima. Huku kaka yake alipatikana bila virusi  Martha alipatwa na virusi

 "Ninakumbu kaka, pacha wangu akinigeukia na kuniambia , 'Hey, ulifanya ngono?' Nilisema, hapana sijui hii imetoka wapi '.."

Mama yake Martha alifariki wakati Martha alipokuwa na umri wa miaka mitano. Alilelewa na baba yake. Wote pamoja walikuwa wanaishi na virusi vya HIV.   

Kati ya ndugu zake wanane alikuwa ni yeye pekee aliyeambukizwa na wazazi wake.

"Kusema ukweli sikuona haja ya kuishi. Vyombo vya habari wakati ule vilikuwa vikitangaza taarifa zinazowanyanyapaa watu. Ulaya HIV ilihusishwa na watu wanaotumia madawa ya kulevya.

Ulaya  ilihusishwa na ngono. Ilinusumbua sana. Nilitaka kujiua."

 Martha alipata faraja katika kuwasaidia vijana wengine wadogo wenye uzoefu sawa na wake  na kujiunga na kikundi cha usaidizi cha HIV.

Martha Clara yuko wazi sana kuhusu hali yake ya HIV na tayari amemfahamisha mpenzi wake yote kuhusu hali yake
Martha Clara yuko wazi sana kuhusu hali yake ya HIV na tayari amemfahamisha mpenzi wake yote kuhusu hali yake
Image: MARTHA CLARA NAKATO

Martha pia anafanya kampeni kuhusu haki za afya hususan kuhusu afya ya ngono na uzazi    

"Wakati unapofanya ngono ya kawaida au kwa usiku mmoja unafurahia wakati kwa usalama. Tumia tu mipira ya kinga ," anashauri. 

Martha anatambua ugumu wa kuwa muwazi kuhusu  HIV. Lakini hamfichi lolote mpenzi wake. 

"Nina uhakika wa asilimia 101 kuwa nitakuwa mama siku moja na mtoto nitakayemzaa, hatakuwa na HIV. Ninasema hilo kwa matumaini yote  niliyonayo moyoni mwangu, kwasababu nimekuwa nikipata dawa zenye ufanisi sana ."

'Sitegemei mengi kutoka kwa jamii'

Lulu Mangang, ni  mwanaume aliyebadili jinsia mwenye umri wa miaka 23 na mwanaharakati wa kampeni dhidi ya Ukimwi mwenye makao yake  katika Imphal, Kaskazini Mashariki mwa India. 

Lulu anasema jamii kila mara itaona ugumu kuwakubali baadhi ya watu
Lulu anasema jamii kila mara itaona ugumu kuwakubali baadhi ya watu
Image: LULU MANGANG

Alisomea masomo ya baiolojia ya wanyama (zoology) na sasa anapanga kufanya masomo ya uzamili ya  bayokemia( biochemistry). "Ningependa kufanya utafiti kuhusu ufanisi wa madawa ya HIV," anasema.

Lulu alizaliwa katika mji wa  Delhi  mwaka  1999  katika familia masikini. Bada ya kifo cha baba yake mwaka 2002, alilelewa na mjomba wake. Anasema  "alipatikana na HIV akiwana umri wa  miaka 6 au 7."

"Sikujua nifanye nini. Nilikuwa mwenye hasira na masikitiko. Ulikuwa ni mchanganyiko wa hisia. Sijui ni nani wa kumlaumu. Nilijikasirikia mwenyewe pia na kujilaani  ."

"Nilizungumza na mama yangu na akaniambia nilipata HIV kutoka kwake ," Lulu anakumbuka

Mama yake alimpeleka katika kikundi cha watoto walioapatwa na maambukizi ya HIV ambacho kilimsaidia Lulu kupata marafiki lakini pia alikabiliwa na ubaguzi.

"Wakati nilipokuwa ninacheza na mtoto  mmoja ghafla nilitaja hali yangu na akaniambia nisimsogelee au kucheza naye. Halafu tuligombana sana ambapo sote tulimia sana."

Lulu anataka kusoma masomo ya bayokemia na kufanya utafiti kuhusu ufanisi wa dawa za HIV
Lulu anataka kusoma masomo ya bayokemia na kufanya utafiti kuhusu ufanisi wa dawa za HIV
Image: LULU MANGANG

Kadri alivyokua, alijifunza jinsi ya kuishi na changamoto. 

Sitegemei mengi kutoka kwa jamii".  Tuko tofauti na sote tuna fikra tofauti."

"Baadhi wanaweza kuniona kama ninavyojiona mwenyewe. Baadhi hawawezi."

Lulu anasema hakuwahi kupata matatizo wakati anapotafuta matibabu kutokana na jinsia yake. Kwa miaka mitatu iliyopita anafanya kazi kama mwanaharakati  katika shirika lisilo la serikali ambalo linamuwezesha kufanya kazi na vijana wenye maambukizi ya HIV.

Lulu anaamini  kuna haja ya kuongeza uelewa ili kuzua ubaguzi   "Kutokana na ukosefu wa kutojiamini na ukosefu wa taarifa watu wengi wanakabiliwa na ubaguzi na kunyanyaswa."

"Niliamua kuwa muwazi kuhusu hali yangu sio kwasababu  inakubalika kiurahisi hapa katika jimbo langu (Manipur).

Mbinu yake ilipokelewa vyema, vijana wengi wanawasiliana naye ili kupata ushauri na usaidizi.      

UKIMWI katika namba   

  • Watu milioni 38.4 kote duniani walikuwa wanaishi na HIV katika mwaka 2021
  • Watu milioni 1. walipatwa na maambukizi mapya ya HIV mwaka 2021 Watu 650 000 [walikufa kutokana magonjwa yanayohusiana na Ukimwi katika mwaka    2021.
  • Idadi hiyo inajumuisha watoto na vijana wenye umri wa kubarehe kote duniani wapatao 110,000   (wenye umri kati ya 0-19 )
  •  Idadi ya vijana wadogo wanaoishi na  HIV wanafikia hadi milioni 2.7  Watoto na vijana wadogo ni  7 % ya watu walioambukizwa virusi vya  HIV lakini  walichukua 17 % ya vifo na  21 % ya maambukizi mapya  katika 2021.
  • Watu milioni 84.2 ndi waliopatwa na maambukizi ya  HIV tangu janga hilo lilipoanza na milioni 40.1 kati yao wamekwishafariki kutokana na magonjwa yanayohusiana na Ukimwi   

Chanzo : UN AIDS na Unicef

'Nitafichua hali yangu ya HIV wakati nitakapokuwa tayari

Ayana,  ni mwanafunzi wa chuo kikuu mwenye umri wa miaka 18 aliyezaliwa katika Osh, Kyrgyzstan. Kwa sasa anaishi katika mji mkuu Bishkek.

Ayana anasema bado hajawa tayari kuwa muwazi kuhusu hali yake ya HIV
Ayana anasema bado hajawa tayari kuwa muwazi kuhusu hali yake ya HIV
Image: UNAIDS

"Tangu nilipojitambua, ninaishi na virusi ," aliiambia  BBC.

Katika mwaka 2006-2007,  watoto 391 walipata maambukizi ya HIV, waliyoambukizwa wakati walipokuwa wakipata matibabu hospitali  akiwemo  Ayana, UNAIDS inasema.

Mama yake Ayana alihudhuria msururu wa semina ambazo zilimsaidia kumlea binti yake bila hofu. 

 Wakati alipokuwa na umri wa kubalehe Ayana alijiunga na makundi ya usaidizi ya HIV.  

"Tunasaidiana. Pia tunazungumzia kuhusu fursa ," anasema.

Kinyume na  Ayana wasichana wengine  hawanywi dawa kila siku, lakini anajaribu kuwasaidia. 

"Nina rafiki ambaye hakutaka kumeza vidonge. Tulibuni maneneo ya siri ya kuwasiliana. Wakati ninapotaka kuwakumbusha rafiki zangu  kuhsuu dawa, nitauliza ulikumbuka kumwagilia maji maua?"

Ayana amefichua hali yake tu kwa familia yake na ndugu wa karibu.   

"Siku moja nitajitokeza wazi, lakini sitafanya hivyo kwa ajili ya wazazi wangu au kwa ajili ya mtu fulani. Nitafanya hivyo wakati niko tayari  ."

Lengo la dunia ni kumaliza maambukizi ya HIV miongoni mwa watoto ifikapo mwaka 2030
Lengo la dunia ni kumaliza maambukizi ya HIV miongoni mwa watoto ifikapo mwaka 2030
Image: GETTY IMAGES

Ayana anasema anafahamu ugumu unaowakabilia marafiki ambao hali yao ilijulikana bila wao kuitangaza.   

"Unyanyapaa na ubaguzi bado upo. Hivi karibuni daftari la  kumbukumbu la rafiki yangu lilichukuliwa na mwanafunzi mwenzake na wakabaini hali yake ya HIV. Taarifa ilisambazwa sana na akakabiliwa na uonevu na hatimaye aliihama shule."

Ayana  amepata nafasi katika chuo kikuu na ana matumaini ya kuwa mwandishi wa habari katika kipindi cha miaka michache. Katika muda ambao hajatingwa na kazi huandika hadithi na ana matumaini kuwa atakuwa na maisha mazuri yajayo. 

"maisha ni kama maji yanayotiririka. Kila kitu kilichotokea kimenifanya niwe nilivyo leo. Ninataka kuendelea kuishi katika maisha haya na nione yananipeleka wapi ."