Hakuna mtu atakayetuyumbisha kuhusu sheria dhidi ya mapenzi ya jinsi moja - Museveni

Yeyote anayepatikana na hatia ya tendo la ngono ya wapenzi wa jinsi moja anakabiliwa na kifungo cha maisha.

Muhtasari
  • Hii inakuja huku kukiwa na shutuma kutoka kwa mataifa ya Magharibi na makundi ya haki za binadamu.

Rais wa Uganda Yoweri Museveni ameelea kuhusu upinzani wa jumuiya ya kimataifa dhidi ya sheria ya kupinga mapenzi ya jinsi moja aliyoitia saini wiki hii.

Bw Museveni alisisitiza kuwa kutiwa saini kwa sheria hiyo ni makubaliano yaliyokamilika, na kukaidi wito wa kutaka ibatilishwe.

"Utiaji saini wa Muswada wa Kupinga mapenzi ya jinsi moja umekamilika, hakuna mtu atakabadilisha hatua yetu. Tunapaswa kuwa tayari kwa vita," alisema katika taarifa yake baada ya mkutano na wanachama wa chama chake cha National Resistance Movement (NRM).

"NRM haijawahi kuwa na lugha mbili, tunachokuambia mchana ndicho tutakuambia usiku," aliongeza.

Hii inakuja huku kukiwa na shutuma kutoka kwa mataifa ya Magharibi na makundi ya haki za binadamu.

Rais wa Marekani Joe Biden aliikosoa sheria hiyo kama "ukiukaji wa kutisha wa haki za binadamu kwa wote" na akatoa wito ifutwe, akiongeza kuwa Marekani inazingatia vikwazo.

Umoja wa Ulaya na mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres pia wamelaani sheria hiyo.

Sheria hiyo ilitiwa saini baada ya bunge kuipuuza - lakini bado ni miongoni mwa sheria kali zaidi za kupinga LGBTQ duniani.

Yeyote anayepatikana na hatia ya tendo la ngono ya wapenzi wa jinsi moja anakabiliwa na kifungo cha maisha.

Sheria pia inatoa hukumu ya kifo kwa "kesi zilizokithiri", ambazo ni pamoja na ubakaji wa mtu aliye na umri wa chini ya miaka 18, au pale ambapo mtu ameambukizwa ugonjwa wa maisha usiopona ikiwa ni pamoja na VVU-UKIMWI.