- "Hatukujua kwanza tatizo lilikuwa nini," Bi Benson alichapisha kwenye ukurasa wa Facebook kuhusu ndege hiyo mwishoni mwa mwezi uliopita.
Shirika la ndege la Air Canada limeomba msamaha baada ya kuwatimua abiria wawili kutoka kwenye ndege kwa kukataa kukaa kwenye viti vilivyokuwa na matapishi.
Susan Benson, ambaye alikuwa kwenye huduma ya Las Vegas-Montreal, alisema rubani aliwaonya abiria kwamba watawekwa kwenye orodha ya kutoruka iwapo wataendelea kulalamika.
Aliongeza kuwa wafanyakazi walijaribu kufunika "harufu mbaya" kwa manukato na kusaga kahawa. Shirika la ndege la Air Canada lilisema kuwa abiria "hawakupata huduma ya kiwango ambacho walistahili kupata".
"Hatukujua kwanza tatizo lilikuwa nini," Bi Benson alichapisha kwenye ukurasa wa Facebook kuhusu ndege hiyo mwishoni mwa mwezi uliopita.
"Inaonekana, kwenye safari iliyotangulia mtu alikuwa ametapika. Mhudumu wa ndege aliomba radhi sana lakini alieleza kuwa ndege ilikuwa imejaa.
" Alisema wafanyakazi "waliweka kahawa ya kusaga kwenye kiti na kupuliza manukato", lakini kwamba kiti na mkanda wa usalama vilikuwa "vimeloa na bado kulikuwa na mabaki ya matapishi yanayoonekana". Bi Benson alisema rubani alitoka kwenye chumba cha marubani baada ya dakika kadhaa.
Abiria waliambiwa "wanaweza kuondoka kwenye ndege... na kupanga safari za ndege kwa gharama zao wenyewe, au wangesindikizwa na usalama na kuwekwa kwenye orodha ya kutosafiri!" Kisha walisindikizwa na usalama.
Air Canada ilisema "inachunguza suala hili zito" na kwamba "taratibu za uendeshaji hazikufuatwa ipasavyo katika tukio hili".