logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanajeshi wa zamani amdunga mkewe mshale jichoni kabla ya kumuibia pesa

Mwanajeshi huyo mpaka wakati taarifa hii inakwenda hewani alikuwa amechimba mitini.

image
na Davis Ojiambo

Habari30 January 2024 - 10:37

Muhtasari


  • • Uchunguzi wa awali umefichua kuwa siku hiyo ya maafa, Ocaya na Onom David walikuwa wakicheza kamari katika duka la mwathiriwa, Apio Grace.
  • • Hata hivyo, Onom alishinda pesa zote, jambo ambalo halikumfurahisha Ocaya.
  •  
Jamaa akirusha mshale

Polisi nchini Uganda wanamsaka mwanajeshi mstaafu mwenye umri wa miaka 53 anayetuhumiwa kumshambulia mkewe na kumchoma mshale katika jicho lake la kulia kalba ya kumuibia.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari kutoka nchini humo, afisa huyo wa zamani kwa jina Owiny Patrick almaarufu Ocaya anashtakiwa kwa kumpiga mkewe, Apio Grace, kwenye jicho lake la kulia kwa upinde na mshale baada ya mzozo wa kucheza kamari.

Katika kisa hicho kilichotokea Januari 24 mwaka huu mwendo wa saa tano usiku, Ocaya anasemekana kumpiga mkewe kwa mshale huo kabla ya kupora KSh42,000 katika duka lake la Kamari.

Uchunguzi wa awali umefichua kuwa siku hiyo ya maafa, Ocaya na Onom David walikuwa wakicheza kamari katika duka la mwathiriwa, Apio Grace. Hata hivyo, Onom alishinda pesa zote, jambo ambalo halikumfurahisha Ocaya.

“Akiwa na wivu na hasira, Owiny alianzisha vita na Onom, akitaka kurejeshewa pesa zake, lakini mke aliingilia kati. Mshukiwa alichukua upinde na mshale, ili kumpiga Ongom David, lakini mkewe alipojaribu kumzuia, alielekeza upinde na mshale kuelekea kwa mkewe na kumpiga jicho la kulia. Alizidi kuiba Ugx 7m, kutoka kwa duka la mkewe na kutoweka nayo,” Msemaji wa Polisi wa Uganda Fred Enanga alinukuliwa.

Mwathiriwa alikimbizwa katika Hospitali ya Abim na baada ya hapo, alipewa rufaa ya Hospitali ya Lacor kwa usimamizi zaidi.

Kwa sasa yuko nje ya hatari. Hata hivyo, mshale huo ulipofusha jicho lake la kulia, baada ya kupenya kwenye tundu la jicho na kubaki pale.

 

"Wote mwathiriwa, watoto wake na jamii wametiwa kiwewe na shambulio hilo," Enanga anakariri kisa hicho.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved