logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mtoto ahofiwa kuliwa na mamba nchini Australia

Mtoto mwenye umri wa miaka 12 alionekana mara ya mwisho jioni ya Jumanne, akiogelea

image

Habari03 July 2024 - 13:30

Muhtasari


  • Eneo hilo ina makadirio ya mamba 100,000 wa maji ya chumvi, zaidi ya mahali pengine popote duniani, lakini mashambulizi si ya kawaida.

Msako mkali unaendelea kaskazini mwa Australia kumtafuta mtoto anayehofiwa kuchukuliwa na mamba.

Mtoto mwenye umri wa miaka 12 alionekana mara ya mwisho jioni ya Jumanne, akiogelea karibu na mji wa mbali wa Nganmarriyanga umbali wa takribani saa 7 kwa gari kuelekea kusini magharibi mwa Darwin.

Polisi wanasema timu ya wataalamu wa utafutaji na uokoaji imetumwa baada ya "ripoti za awali kusema mtoto huyo alishambuliwa na mamba".

Eneo hilo ina makadirio ya mamba 100,000 wa maji ya chumvi, zaidi ya mahali pengine popote duniani, lakini mashambulizi si ya kawaida.

Wanajamii huko Nganmarriyanga, hapo awali ilijulikana kama Palumpa na makazi ya watu 364 pekee na polisi wa eneo hilo walianza kumtafuta mtoto huyo mara baada ya kutoweka mwendo wa 17:30 saa za ndani (08:00 GMT).

Sasa wameunganishwa na maafisa wa ziada na timu ya utaftaji na uokoaji wa kitaalamu ambao wanatafuta nchi kavu na majini.

Utafutaji wa angani unaweza pia kuanza, kulingana na vyombo vya habari vya ndani.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved