Mwanafunzi awashtaki walimu kadhaa kwa unyanyasaji wa kijinsia

Alisema hata baada ya kulifikisha suala la unyanyasaji wa kijinsia na unyanyasaji wa walimu kwa uongozi, hakuna kilichofanyika.

Muhtasari
  • Alipata michubuko kutokana na kipigo na mikono yake ilikuwa imevimba zaidi akisema alikuwa anaumwa na hakuhudumiwa kimatibabu na shule
Mahakama
Mahakama
Image: MAHAKAMA

Mwanafunzi wa kidato cha 3 katika Shule ya Upili ya Wasichana ya Kereri  Kisii ameishtaki shule hiyo akiwashutumu walimu kadhaa kwa unyanyasaji wa kijinsia.

Katika ombi lililowasilishwa katika mahakama ya Nairobi, msichana ambaye ameshtaki kupitia kwa mamake alisema shule hiyo inajulikana kwa unyanyasaji wa kijinsia na walimu wa kiume.

Alisema hata baada ya kulifikisha suala la unyanyasaji wa kijinsia na unyanyasaji wa walimu kwa uongozi, hakuna kilichofanyika.

Wameshtaki mwalimu mkuu wa shule Teresa Atieno Otieno na walimu saba kwa makosa yanayodaiwa.

Alisema unyanyasaji huo ulianza kati ya Juni 7 na 14, 2020, wakati jina lake lilipotajwa kuwa mmoja wa wapiga kelele na mkuu wa darasa.

Alisema mwalimu wa kiume alikwenda darasani na kutumia orodha ya wapiga kelele kuwachapa viboko wanafunzi.

"Nilimsihi asinipige viganja vyangu vya mikono ambavyo aliviondoa na akaendelea kunichapa viboko vikali huku akiniambia kuwa mimi sio maalum" zinasomeka karatasi za mahakama.

Alipata michubuko kutokana na kipigo na mikono yake ilikuwa imevimba zaidi akisema alikuwa anaumwa na hakuhudumiwa kimatibabu na shule.

Msichana huyo alisema mwalimu yuleyule alienda darasani kwake siku iliyofuata akiwa na maji  moto na akajitolea kukanda mkono wake uliokuwa umevimba. Anadai kwamba alimkuta akiwa ameketi peke yake na ndipo alipomfanyia ngono.

“Unajua wewe ni msichana mrembo sana, nitakununulia gifts… na nikupe pesa kwa wiki ukikubali tu-have sex nataka tupate mtoi ukimaliza shule,” zilisoma hati za korti.

Alimweleza mamake ambaye kisha aliamua kumpeleka katika Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Kisii ambapo picha ya X-ray ilifanywa mkononi mwake na kuwekewa kombeo.

Alisema mapema mwaka huu alipata unyama na mwalimu huyo ambaye alimpiga kofi usoni alipomkuta amelala kwenye meza yake saa 4 usiku.

Mama na binti wanatafuta fidia kwa sababu ya mateso ya kimwili na kiakili, uchungu, na mateso.

Mwaka jana alisema mwalimu wa pili alimnyanyasa kingono kwenye chumba cha wafanyakazi.

"Kisha aliendelea kuweka mkono wake kwenye paja langu na kunipapasa paja la ndani alipokuwa akielezea kuhusu kufanya hivyo katika shule ya upili kisha akajiondoa," alisema.

Kulingana na karatasi za mahakama, walimu zaidi wa kiume waliruhusiwa kukaa katika vyumba vilivyo karibu na bweni hilo licha ya shule hiyo kuwa na sehemu nyingine kuelekea mashamba ambayo yanakaliwa na walimu wa kike.

Anadai kuwa mmoja wao, mwalimu wa kiume angetumia njia iliyo karibu na eneo la wazi ambapo wasichana wangeoga saa kumi asubuhi.

"Alikuwa na tabia ya kipekee ya kuelekeza mwanga kutoka kwa mwenge wake kuelekea wasichana ambao wakati huo walikuwa wakioga katika eneo la wazi kando ya njia alipokuwa akitembea kutoka kwa makao ya mwalimu" zilisoma karatasi za mahakama.

Pia amedai kuwa wakati fulani mwalimu huyu alinaswa na wanafunzi akimbusu mwanafunzi karibu na mabweni na kulikuwa na ghasia shuleni huku wasichana wakiandamana.

Mama huyo anasema unyanyasaji wa kingono na unyanyasaji wa watoto katika shule hiyo uliripotiwa kwa DCI mwezi Machi.