Mahusiano

Unayofaa kujua kabla ya kuanza mahusiano na mwanamume mwenye uhusiano wa karibu na mamake

Mtu wa kwanza kumkimbilia ni mamake

Muhtasari
  • Mama’s boy hufuata kila wanachoambiwa na mama yao na wakati mwingi hilo huvuruga  uhusiano wao na wapenzi wao au hata rafiki zao.
  • Kila mtu ana udhaifu wake lakini kwa mama’s boy –mamake ni malaika, anayajua yote na hawezi katu kukosolewa.

 

Diamond na Tanasha

Umeyaskia mengi kuhusu msemo huo wa wanaume ambao kila linalosemwa na mama yao ni sheria na hivyo basi  kauli za mama zao hutawala maisha yao kuanzia kila uamuzi wanaofanya.

Imekuwa vigumu kwa wanawake wengi kuwa katika uhusiano wa kudumu na wanaume ambao huitwa mama’s boy kwa sababu wakati wote lazima kivuli cha mama yao kiwe nyuma yako. Kama Diamond Platinumz wa Bongo, imefahamika kwamba mahusiano yake na  msururu wa wanawake wote hao umekuwa  ukivurugwa na muingilio wa mamake  Sandra Dangote

Mama’s boy hufuata kila wanachoambiwa na mama yao na wakati mwingi hilo huvuruga  uhusiano wao na wapenzi wao au hata rafiki zao. Sasa hizi hapa baadhi ya ishara za kujua kwamba mwanamme ambaye upo katika mahusiano naye ni mama’s boy na wakati wote itakuwa ni ushindani kati yako na mamake.

 

 Mtu wa  kwanza kumkimbilia ni mamake

Akiwa na tatizo hivi basi mtu wa kwanza kujua ni mamake. Iwapo ana habari njema za kusema basi fahamu kwamba mamake ndiye atakayekuwa wa kwanza kujuzwa hata akiwa na mke, anachosema mamake ni sheria, anachopinga mamake basi ni mwiko

 Wanapenda kuishi na mama yao

Kuna sababu nyingi za mtu  mzima anayejiweza kutaka kuishi na mamake kwa mfano iwapo mama  ni mgonjwa au wataka kuokoa fedha kwa kuepuka kulipa kodi lakini mama’s boy ataishi na mamake hata iwapo ana miaka 40 na zaidi. Wakati mwingi hana haraka ya kuhamia kwake na isitoshe mamake ndiye humfulia nguo.

 Huwezi kumkosoa mamake

Kila mtu ana udhaifu wake lakini kwa mama’s boy –mamake ni malaika, anayajua yote na hawezi katu kukosolewa. Ukitilia doa mamake basi wewe utakuwa  adui mkubwa. Hata iwapo mamake ana kosa na ni la wazi, utafanya kosa kubwa sana kwa mama’s boy kumkosoa mamake.

  Mama ndiye jaji mkuu

 

Maamuzi muhimu ya kibinafsi hata yanayomhusisha mkewe yatafanywa na  mama mtu. Ataamua wajukuu wake wataenda shule gani, mtajenga nyumba aina gani, shamba mtanunua wapi na hata  siku ya krisimasi mtapika nini …Ataamua hata wakati wa kumpata mtoto mwingine au  ni  njia gani ya kupanga uzazi unayofaa kutumia ..

Kuishi katika boma moja na mama mkwe  ambaye uhusiano wake na mwanawe ni wa chanda na pete ni kama kuishi jela kwa baadhi ya wanawake. Huna uhuru .

Kwa mfano, wakati Diamond alipokuwa pamoja na Tanasha, Mama Dangote  alikuwa akidhibiti kila hali ya maisha yao. Tanasha amesema wakati mwingine aliamua kujituliza kama mkaza mwana mwema kwa kunyamza lakini hilo kwa kweli halikumsaidia.

Zari  naye pia alizingumza tabia hiyo ya mama Dangote kuingilia kabisa maisha ya kibinafsi ya Diamond lakini wengi walifikiri kwamba labda Zari alikuwa na machungu baada ya kutengana na msanii huyo.

Iwapo bado wataka au upo katika uhusiano na mama’s boy basi jitayarishe kwa msururu wa kesi ambazo utashindwa wakati mwingi.