Masaibu

Mwalimu aliyekuwa akiwazuia wanafunzi wake bangi agundulika

Hakuna aliyeamini kwamba mwalimu huyo mpole na chapakazi alikuwa na ukatili wa kuwauzia wanafunzi wake dawa za kulevya akijua fika madhara yake.

Muhtasari
  • Jared   Akitoto alikuwa amejiundia pesa kwa muda mrefu na sio kupitia kazi yake ya ualimu bali kuwauzia wanafunzi wake bangi kutoka nchi jirani ya Uganda .
  • Chini ya uchapoakazi wake na upole ambao mwalimu  Jared alikuwa nao,kulikuwa na siri kubwa ambayo ni wanafunzi watundu waliokuwa wakitumia dawa za kulevya ndio waliofahamu . 
Mfanyikazi adondoa bangi katika kituo cha utafiti/ Maktaba
Mfanyikazi adondoa bangi katika kituo cha utafiti/ Maktaba

 

Shule moja ya upili huko Malaba miaka kadhaa iliyopita ilijipata katika vyombo vya habari kwa sababu  zisizokuwa nzuri .Hii ni baada ya  kulipuka kwa  kava  ya mwalimu mmoja aliyekuwa ameandikwa kazi na bodi ya  usimamizi wa shule aliyekuwa akiwauzuia wanafunzi mihadarati na hasa bangi.

Jared   Akitoto alikuwa amejiundia pesa kwa muda mrefu na sio kupitia kazi yake ya ualimu bali kuwauzia wanafunzi wake bangi kutoka nchi jirani ya Uganda . Alikuwa ameweka mikakati kabambe ya  kuzuia kugunduliwa na waliokuwa wakimjua baadaye hawakuamini alipokamatwa kwa hatia hiyo kwani licha ya mkuwa mwalimu chapa kazi ,alikuwa pia amejituma kuwasaidia wanafunzi wake kwa mafunzo  ya mambo kama  michezo  na hata aliiongoza timuya shule hiyo katika mashindano ya kanda na wakafika kiwango cha mikoa . Chini ya uchapoakazi wake na upole ambao mwalimu  Jared alikuwa nao,kulikuwa na siri kubwa ambayo ni wanafunzi watundu waliokuwa wakitumia dawa za kulevya ndio waliofahamu .  Jared  alikuwa ameunda mtandao wa ushirikiano shuleni humo ambapo  angezileta dawa za kuleya  zilizohifadhiwa shuleni .Miongoni mwa waliomsadia kuziuza dawa hizo ni wapishi wa shule na hata  wafanyikazi waliokuwa wakiingia na kutoka mle shuleni .

 

Shehena kubwa ya bangi ingeletwa kutoka Uganda hadi kwake ,kisha aangeipakia katika misokoto na kisha kuipeleka shuleni ambapo wapishi wangemsaidia kuificha .baadaye bangi hiyo ingeuzwa kwa wanafunzi wakati wa usiku na hata  wakati wa  shughuli za michezo au safari za nje ya shule ,kungekuwa na  wakala wake miongoni mwa wanafunzi ambaye angeendelea kuziuza dawa za kulevya kwa wanafunzi wa shule jirani na hata watu wa   nje .

Palipotokea ripoti kwamba wanafunzi wa shule hiyo walikuwa wakitumia bangi na visa vya utovu wa nidhamu  kuongezeka ,mwalimu mkuu alishangaa wanafunzi  wake  walikuwa wakitoa wapi bangi . Uchunguzi wa  kisiri ulianzishwa na  shule na hata kuwahusisha polisi . Wakati wapishi wawili walipokamatwa  wakiwa na misokoto ya bangi ,siku ya 40 kwa mwalimu Jared ilikuwa imekaribiwa.walihojiwa na kutakiwa kusema wote waliohusika na biashara ya mihadaratai shuleni . Walipomtambua mwalimu Jared kama kiongozi wa mtandao wa uuzaji wa mihadarati ,kila mmoja shuleni humo aliachwa kinywa wazi .

Hakuna aliyeamini kwamba mwalimu huyo mpole na chapakazi alikuwa  na ukatili wa kuwauzia wanafunzi wake dawa za kulevya akijua fika madhara yake. Jared alikamatwa  na polisi walipomfikisha kwake ,shehena ya dawa za kulevya  walizopata  iliwashangaza. Mwalimu Jared alishtakiwa na kufungwa jela ,tamaa yake ya kutengeza pesa kwa kuhatarisha maisha ya wanafunzi ikaishia kumuacha bila kazi ya ualimu na majuto chungu nzima .