Semi maarufu za hayati Mwai Kibaki zilizowafurahisha wakenya

Muhtasari
  • Semi maarufu za hayati Mwai Kibaki zilizowafurahisha wakenya
Rais mstaafu Mwai KIbaki
Image: FREDRICK OMONDI

Huku wakenya wakiendela kutuma riasala za rambi rambi kwa familia ya rais mstaafu Mwai Kibaki, nyakati zake katika uongozi hazijasaulika.

Kibaki alikuwa rais wa tatu wa jamhuri ya Kenya.

Semi maarufu zilizofahaika na wakenya, kutoka kwa rais huyo ni pamoja na;

  1. Bure kabisa
  2. Mafi ya kuku
  3. Kumbafu
  4. Wachana nayooo
  5. Ni utoto
  6. Hapanaaaa
  7. Sio lazimaaaa
  8. ooh yes
  9. Kula pombe
  10.  What the hell’
  11.  Anyway

Kabla ya kuwa rais Kibaki alikuwa amehudumu kama makamu wa rais na waziri katika serikali ya hayati rais Daniel Arap Moi.

Katika hotuba yake rais Kenyatta alimpongeza Kibaki kwa kubadilisha uchumi wa Kenya uliyokuwa umedorora.

Hayati rais Kibaki hajaonekana kwenye umma kwa muda mrefu huku mara ya mwisho ikiwa wakati wa maombolezo ya kifo cha hayati rais Daniel Moi mwezi Februari 2020.

Marehemu kibaki alizaliwa mwaka 1931 katika eneo la Gatuyaini, Nyeri. Alisomea shule ya upili ya Nyeri na kujiunga na shule ya Mangu kwa elimu ya kidato cha tano na sita kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Makerere.