logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mombasa: Mtoto wa miaka 14 atekwa nyara na kuuawa kwa kucharangwa mapanga

Kennedy mulani mwenye umri wa miaka kumi na 14 kuuwawa na magenge wenye silaya  Mombasa.

image
na Davis Ojiambo

Habari08 September 2023 - 09:16

Muhtasari


  • • Siku ya Alhamisi mwili wake ulisafirishwa hadi nyumbani kwa  babu yake Masogalini kata ndogo ya Kibwezi mashariki kwa mazishi
Kisu cha mauaji

Familia moja katika kaunti ya Mombasa inalilia haki kutendeka baada ya mtoto wao wa miaka 14 kutekwa nyara na watu wasiojulikana kisha baadae mwili wake kupatikana ukiwa umecharangwa mapanga.

Kennedy Maluni, kijana mwenye umri wa miaka 14 ambaye alikuwa mtahiniwa wa mwaka huu katika mtihani wa KCPE alikuwa ametumwa na mamake dukani majira ya saa mbili usiku lakini hakuwahi rejea nyumbani hadi pale mwili wake ulipopatikana umekatwa katwa kwa panga siku chache baadae.

 

Siku ya Alhamisi mwili wake ulisafirishwa hadi nyumbani kwa  babu yake Masogalini kata ndogo ya Kibwezi mashariki kwa mazishi

Kennedy alikatwakatwa na panga na majambazi Mwamlai,kaunti ndogo ya jomvu Mombasa tarehe 23 Agosti

Mamake mzazi Margret Mbithe alisema kuwa alitarajia kuwa katika umri wake wake wa uzee mtoto wake Kennedy angemusaidia ila imebaki kuwa kilio kwake kwa kuwa watu ndio wanamusaidia ikiwemo kampuni ya usambazaji saruji ya Mombasa ndio inamusaidia kurudisha mwili wa mtoto wake nyumbani.

Mbithe anasema kuwa hatapumuzika mpaka pale waliotekeleza kitendo hicho cha unyama kwa mwanawe watakapotiwa hatiani na kuhukumiwa.

Walimu katika shule ya Vision of Hope Educational Center walimtaja Kennedy kama mwanafunzi aliyetia bidii kwa masomo yake.

Alhamisi wanaharakati wa haki za binadamu ,makasisi,na mabalozi wa haki za watoto walisema kuwa Kennedy anafaa kupata haki huku wakiomba  polisi kuchunguza kisa hicho na kuwatia mbaroni wote na ambao waliusika na kifo cha mtoto mdogo wa shule kwa kukatisha uhai wake .

Mkuu wa polisi wa jomvu Lydia Wanjiru amesema kuwa maafisa wa upelelezi wamewakamata watu watatu wanaosaidia upelelezi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved