Muhtasari
•Benson Njiru (22) na Emmanuel Mutura (19) ambao walikuwa wanafunzi katika chuo kikuu cha Kabarak na chuo cha mafunzo ya kiteknolojia cha Don Bosco mtawalia wanadaiwa kukamatwa na polisi kutoka kituo cha polisi cha Manyatta mnamo Jumapili.
•Kwa siku tatu walitafutwa kila mahali walikodhaniwa kuwa ikiwemo kwa kituo cha polisi cha Manyatta ila juhudi zote ziliangulia patupu.
•Siku ya Jumatano wazazi hao waliandamana na kikundi kikubwa cha wanakijiji waliokuwa wamejawa na ghadhabu na kushambulia kituo cha polisi cha Manyatta wakidai majibu kuhusiana na kifo cha watoto wao.