Balozi wa Kenya nchini Namibia ameshambuliwa mtandaoni baada ya picha inayomuonesha akiwa karibu na swara aliyeuawa akiwa na bunduki mkononi kusambaa katika mitandao ya kijamii.
Benjamin Langat, ambaye hajatoa tamko lolote kuhusu picha hiyo , ametuhumiwa na baadhi ya watumiaji wa mtandao wa Twitter kwa kukiuka kujitolea kwa Kenya kwa uhifadhi wa wanyamapori licha ya kupata ruhusa ya kuwinda nchini Namibia::
Even with the legal practice Namibia has on game hunting practice…for a Kenyan Ambassador Hon Benjamin Langat to participate… he violates his country policy and its commitment which Kenya leads in wildlife conservation and advocate for non Consumptive practices. SHAME ON YOU pic.twitter.com/lgQZ2lAQx2
— 🐬 𝒦𝒶𝓇𝑒𝓃 𝒦 𝒦𝓃𝒶𝓊𝓈𝓉 🐬 (@Karimi_Karen) August 30, 2021
Wengi walitoa maoni juu ya kejeli ya picha hiyo kwenye chapisho la Ikulu kuhusu rais akipongeza mashirika ya wanyama pori ya Kenya kwa juhudi zao za kupambana na uwindaji haramu- mtumiaji mmoja wa twitter alitoa wito wa balozi huyo kurejeshwa nyumba:
Kenya ili piga marufuku uwindaji haramu mwaka 1977 ili kuhifadhi wanyamapori wake.
Namibia inaruhusu uwindaji wanyamapori na kutumia fedha hizo kuhifadhi wanyama wanaokabiliwa na tisho la kuangamia