Virusi vya Covid huenda viliwaua wahudumu wa afya kati ya elfu 80 hadi 180-WHO

Vifo hivyo vilitokea kati ya Januari 2020 na Mei mwaka huu.

Image: GETTY IMAGES

Virusi vya Covid 19 vimeathiri vibaya wafanyikazi wa huduma ya afya na huenda viluwaua kati ya 80,000 na 180,000, Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) linasema.

Wafanyakazi wa huduma ya afya lazima wapewe kipaumbele kwa chanjo, mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus alisema

Vifo hivyo vilitokea kati ya Januari 2020 na Mei mwaka huu.

Hapo awali, afisa mwingine mwandamizi wa WHO alionya ukosefu wa chanjo unaweza kuona janga hilo likiendelea hadi mwaka ujao.

Kuna takriban wafanyakazi milioni 135 wa huduma za afya ulimwenguni.

"Takwimu kutoka nchi 119 zinaonyesha kuwa kwa wastani, wafanyikazi wawili kati ya watano wa huduma za afya ulimwenguni wamepewa chanjo kamili," Dk Tedros alisema.