- DP William Ruto amemsuta kiongozi wa Wiper Kalonzo kwa kumuunga mkono kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga kuwania urais
DP William Ruto amemsuta kiongozi wa Wiper Kalonzo kwa kumuunga mkono kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga kuwania urais.
"Mimi sina shida na mtu yeyote, nilisaida Raila hadi akawa Prime Minister lakini ilifika wakati nikagundua hapendi Mungu nikachoka nikamwachia Kalonzo
Kalonzo alimsukuma hadi siku hizi nywele yake imekwisha. Ukipata mtu analalamika juu ya Kanisa, jua kuna shida," Ruto alisema.
Ruto alidai kuwa Raila hawezi kushinikizwa kuwa rais zaidi.
"Niko hapa ili yeye(Raila) asije kukusumbua," alisema huku akicheka.
Ruto zaidi alimwambia Raila aepuke ghasia kabla ya uchaguzi wa Agosti 9.Aliwataka washindani wake kutoendelea kutoa visingizio kuhusu vurugu.
"Ninataka kuwahimiza washindani wangu kuhakikisha kuwa katika mlingano wetu wa uchaguzi hakuna vurugu," Ruto alisema.