logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maafisa 5 wa polisi wa SSU watazuiliwa hadi Jumatatu - Mahakama

Watano hao wamefikishwa mahakamani kuhusiana na kutoweka kwa raia wawili wa India na dereva wao.

image

Habari27 October 2022 - 11:00

Muhtasari


  • Hakimu mkuu wa mahakama ya Kahawa aliamuru kwamba ataamua Jumatatu ikiwa watano hao watazuiliwa kwa siku 30 zaidi zilizoombwa na serikali kuruhusu uchunguzi ufaanyike

Maafisa watano wa polisi kutoka kitengo cha SSU kiliyovunjiliwa mbali na Rais Ruto watazuiliwa katika kituo cha polisi cha Industrial area  hadi Jumatatu watakapofikishwa mahakamani tena.

Hakimu mkuu wa mahakama ya Kahawa aliamuru kwamba ataamua Jumatatu ikiwa watano hao watazuiliwa kwa siku 30 zaidi zilizoombwa na serikali kuruhusu uchunguzi ufaanyike.

Watano hao wamefikishwa mahakamani kuhusiana na kutoweka kwa raia wawili wa India na dereva wao.

Mahakama itaunganisha kesi na ya maafisa wengine 4 waliofikishwa mahakamani awali kuhusiana na suala sawa.

Wakili wao Danstan Omari alidai kwamba wateja wake waliteswa walipokuwa kizuizini katika kituo cha polisi cha Industrial area.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved