Nairobi: Mhudumu wa M-Pesa apigwa risasi tumboni na mkononi na kuibiwa Ksh 70K

Opati alipiga kelele kuomba msaada na kusababisha genge hilo kufyatua risasi na kumpiga risasi tumboni na mkono wa kushoto.

Muhtasari

• Genge hilo lilidai kwa mtutu wa bunduki kwamba asalimishe mali zake zote za thamani zikiwemo pesa taslimu.

• Maafisa katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta walisema alilazwa akiwa katika hali nzuri.

Mwanafunzi ajiua kwa kujipiga risasi Kilimanjaro
Mwanafunzi ajiua kwa kujipiga risasi Kilimanjaro
Image: YoutubeScreengrab

Mhudumu wa M-Pesa alipigwa risasi na kujeruhiwa vibaya kabla ya kuibiwa Sh70,000 katika eneo la Highrise Nairobi.

Jacob Aoko Opati, 26, alipigwa risasi tumboni na mkononi na anapigania maisha yake hospitalini kufuatia shambulio hilo.

Aliwaambia polisi kwamba alikuwa akielekea nyumbani Ijumaa usiku kutoka kwa duka lake la Mpesa eneo la Soweto alipokabiliwa na watu wawili wenye silaha.

Genge hilo lilidai kwa mtutu wa bunduki kwamba asalimishe mali zake zote za thamani zikiwemo pesa taslimu.

Opati alipiga kelele kuomba msaada na kusababisha genge hilo kufyatua risasi na kumpiga risasi tumboni na mkono wa kushoto.

Genge hilo lilinyakua pesa alizokuwa nazo na kitambulisho chake cha kitaifa na kutokomea kwenye kitongoji duni.

Polisi walitahadharishwa na kukimbia katika eneo la tukio kabla ya kusaidia kumpeleka Opati hospitalini.

Maafisa katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta walisema alilazwa akiwa katika hali nzuri.

Polisi walisema bado hawajakamatwa kuhusiana na ufyatuaji risasi na wizi lakini msako mkali dhidi ya genge hilo unaendelea.

Visa vya ujambazi wa kutumia silaha vimeongezeka huku polisi wakijitahidi kudhibiti hali hiyo.