logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mahakama yatupilia mbali amri ya kufungwa kwa akaunti za benki za msajili mkuu wa mahakama Ann Amadi

Ann Amadi amepata afueni baada ya mahakama kuu kufutili mbali amri iliyofungia akaunti zake za benki.

image
na Davis Ojiambo

Habari09 June 2023 - 10:05

Muhtasari


  • • Hata hivyo, hakimu alitupilia mbali maombi ya Amadi ya kufuta mbali kesi dhidi yake na wengine wawili - Brian Ochieng na wakili mwingine.

Msajili Mkuu wa mahakama Ann Amadi amepata afueni baada ya mahakama kuu kutupilia mbali amri ya kufungwa kwa akaunti zake za benki.

Jaji Alfred Mabeya ameamua kuwa hakuna ushahidi unaoonyesha kuwa Amadi ilinufaika na dola milioni 100 zinazodaiwa kulipwa na kampuni moja ya Dubai kwa ununuzi wa dhahabu.

"Hakuna chochote kinachoonyesha kuwa mshtakiwa wa kwanza (Amadi) alihusika katika shughuli za kila siku za kampuni ya mawakili au ushahidi wa kuonyesha kwamba alinufaika na fedha hizo," mahakama ilisema.

Jaji Mabeya alisema mwanawe Brian Ochieng anafaa kubeba msalaba wake mwenyewe kwa sababu yeye ni mtu mzima na Amadi kuwa mamake haimaanishi kwamba analazimika kubeba mzigo huo kwa niaba yake.

Hata hivyo, hakimu alitupilia mbali maombi ya Amadi ya kusitisha kesi dhidi yake na wengine wawili - Brian Ochieng na wakili mwingine.

Hakimu alisema Amadi atasalia kuwa mshtakiwa katika kesi hiyo kwani Demetrios Bradshaw alikuwa sawa kisheria kumshtaki ili kuonyesha kwamba kampuni ya mawakili imesajiliwa kwa jina lake.

Katika kesi hiyo, Amadi, mwanawe Ochieng, rais wengine wawili wa Kenya na mmoja wa  Liberia wameshtakiwa na Bruton Gold Trading LLC, kwa madai kwamba kampuni hiyo ilipoteza dola 742,206.

Kampuni hiyo inadai kuwa pesa hizo zilikusudiwa kununulia dhahabu ambazo hazikufikishwa kwao Dubai.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved