logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ndugu wawili wadaiwa kumuua mpenzi wa mama yao Embu

Polisi walisema msako wa kumtafuta mshukiwa mwingine unaendelea.

image

Habari05 September 2023 - 16:21

Muhtasari


  • Peter Mwangi aliaga dunia baada ya kupigwa na wanaume wawili waliomshtumu kwa kujaribu kuchukua familia yao.
crime scene

Katika kijiji cha Kiambere, Kaunti ya Embu, mwanamume mwenye umri wa miaka 45 aliuawa katika boma ambalo alikuwa ameenda kumuona anayedaiwa kuwa mpenzi wake.

Peter Mwangi aliaga dunia baada ya kupigwa na wanaume wawili waliomshtumu kwa kujaribu kuchukua familia yao.

Polisi walisema marehemu alikuwa ameenda kukutana na mpenzi wake mwenye umri wa miaka 50 ambaye ni mama wa wanaume hao wenye umri wa miaka 20 na 23 wakati mapigano yalipozuka.

Wanaume hao waliamuru marehemu kuondoka nyumbani kwa mama yao na kusababisha mapigano ambayo yaligeuka kuwa mbaya.

Mmoja wa wanaume hao alikamatwa baadaye huku mwingine akitoroka baada ya tukio la Jumatatu, Septemba 4.

Polisi walisema msako wa kumtafuta mshukiwa mwingine unaendelea.

Mwili huo ulihamishwa hadi kwenye chumba cha kuhifadhia maiti ukisubiri uchunguzi wa maiti.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved