logo

NOW ON AIR

Listen in Live

IPOA yalaani vikali shambulio la afisa wa polisi Kasarani

Alisema maafisa wa Ipoa wametembelea eneo la tukio na kuwahoji mashahidi kadhaa.

image

Habari03 June 2024 - 14:00

Muhtasari


  • Mwenyekiti wa Ipoa Anne Makori alisema Jumatatu afisa huyo wa polisi, Koplo Jacob Ogendo, alikuwa katika zamu ya usimamizi wa trafiki katika barabara ya Kamiti huko Kasarani aliposhambuliwa.

Mamlaka Huru ya Uangalizi wa Polisi imekashifu kisa ambapo dereva mmoja alimshambulia afisa wa polisi huko Kasarani siku ya Jumapili.

Mwenyekiti wa Ipoa Anne Makori alisema Jumatatu afisa huyo wa polisi, Koplo Jacob Ogendo, alikuwa katika zamu ya usimamizi wa trafiki katika barabara ya Kamiti huko Kasarani aliposhambuliwa.

"Ipoa inabainisha kuwa washukiwa waliohusika wote wako chini ya ulinzi wa polisi kwa sasa," Makori alisema kwenye taarifa.

Alionyesha wasiwasi wake juu ya shambulio hilo, akisema vitendo kama hivyo vinazuia utoaji wa huduma za usalama na kudhoofisha utawala wa sheria.

Makori aliendelea kusema kuwa vitendo hivyo vya uvunjaji sheria vinasumbua umma haki yao ya kikatiba ya kufurahia huduma bora ya polisi.

"Ipoa inawataka Wakenya wanaohisi kutoridhika na huduma za polisi au maafisa wa polisi kuwasilisha malalamishi yao kwa Mamlaka ili uchunguzi ufanyike kupitia nambari ya bila malipo 1559 badala ya kukimbilia kushambulia polisi," alisema.

Makori aliendelea kusema kuwa Mamlaka imeanzisha uchunguzi kuhusu kifo cha kusikitisha cha mtoto ambaye alikuwa chini ya ulinzi wa polisi katika Kituo cha Polisi cha Kambuu kaunti ya Makueni.

Alisema maafisa wa Ipoa wametembelea eneo la tukio na kuwahoji mashahidi kadhaa.

Makori alisema uchunguzi huo unalenga kufichua mazingira yaliyosababisha kifo cha mtoto huyo.

"Baada ya kukamilika kwa uchunguzi, na pale ambapo hatia ya jinai imezuiliwa Ipoa itapendekeza kufunguliwa mashitaka," alisema.

Mtoto huyo alikuwa kituoni ambapo mamake Zipporah Mutheu alizuiliwa

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved