logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto aeleza nia ya kujadiliana na vijana kwenye X space

Rais Ruto ameelezea nia yake ya kujihusisha kwenye mazungumzo na vijana kwenye mtandao wa X

image
na Davis Ojiambo

Habari01 July 2024 - 07:07

Muhtasari


  • •Hii inafuatia wito wa wakenya, haswa Gen Z, kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, ambao wamesema kwamba ikiwa mazungumzo yoyote yatafanyika, yafanywe kwenye X space.
  • • Katika mahojiano na wanahabari Jumapili, Rais alisema yuko tayari kujadili masuala yoyote ambayo wanaweza kuwa nayo.

Rais William Ruto ameelezea nia ya kuwashirikisha vijana kwenye mtandao wa X kwenye mazungumzo kuhusu masuala yanayowakumba.

Hii inafuatia wito wa wakenya, hasa Gen Z, kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, ambao wamesema kwamba ikiwa mazungumzo yoyote yatafanyika na serikali, yafanywe kwenye 

Katika mahojiano na wanahabari siku ya Jumapili, Rais alisema yuko tayari kujadili masuala yoyote ambayo wanaweza kuwa nayo.

“Nasikia vijana wanasema hawataki jukwaa  la wadau wengi ,labda tufanye mazungumzo na rais kwenye X. Mimi niko wazi kufanya mazungumzo na vijana kwenye jukwaa wanalostarehe nalo. Wakitaka nishirikiane nao kwenye X, nitakuwepo," Rais Ruto alisema.

Aliongeza, "Nataka tujadili kuhusu kodi, nataka tujadili ukosefu wa ajira, rushwa na masuala yote."

Vijana wamekuwa wakiandaa maandamano nchini kote kwa muda wa wiki mbili kuhusu mswada wa fedha wa 2024, ambao Ruto aliondoa kufuatia shinikizo iliyoongezeka.

Hata hivyo,rais  alithibitisha ufahamu wake kuhusu changamoto za vijana na kuahidi kushughulikia matatizo yao kwa kina.

"Nina vijana nyumbani, na ninajua wasiwasi wao," alisema.

Jukwaa la X Space hivi majuzi limekuwa na shughuli kali, huku vijana wakilitumia kutoa maoni yao kwenye X Space, ambayo wanataka rais ashughulikie.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved