logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi wamuokoa mshukiwa wa wizi kutokana na kuuawa na waandamanaji Mombasa

Hata hivyo anakamatwa tena na kupigwa kabla ya polisi kuingilia kati na kumuokoa.

image

Habari02 July 2024 - 13:04

Muhtasari


  • Hii ilikuwa baada ya kudaiwa kunaswa na waandamanaji wanaoipinga serikali mjini Mombasa akijaribu kuiba.

Polisi mjini Mombasa mnamo Jumanne waliingilia kati kumwokoa mshukiwa wa mwizi kutokana na kuuawa.

Hii ilikuwa baada ya kudaiwa kunaswa na waandamanaji wanaoipinga serikali mjini Mombasa akijaribu kuiba.

Katika video, mwanamume huyo aliyevalia shati jeusi anaonekana akipigwa na waandamanaji kabla ya kutoroka.

Hata hivyo anakamatwa tena na kupigwa kabla ya polisi kuingilia kati na kumuokoa.

Kisha mshukiwa anaokolewa na maafisa wa polisi waliomchukua kwa land cruiser na kuondoka naye.

Maandamano yalianza mapema mjini Mombasa huku waandamanaji wa amani wakiimba nyimbo za kuipinga serikali na kubeba mabango.

Wakati fulani, vikundi vya waandamanaji wa amani mjini Mombasa vilijigawanya katika makundi mawili huku wahuni wakijinufaisha na kuanza kuwahangaisha waandamanaji.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved