logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Afisa wa polisi mafichoni baada ya kudaiwa kumdunga kisu mkewe Siaya

Mkuu wa polisi wa kaunti hiyo alifichua kuwa mwathiriwa yuko katika hali nzuri

image

Habari09 July 2024 - 11:08

Muhtasari


  • Kulingana na kamanda wa polisi kaunti ya Siaya Cleti Kimaiyo, afisa huyo wa CIPU alizua ugomvi na mkewe na kumdunga  kisu upande wa kushoto wa tumbo kabla ya kutoweka gizani.
crime scene 1

Afisa wa polisi anayehusishwa na Kitengo muhimu cha Ulinzi wa Miundombinu (CIPU) amejificha baada ya kudaiwa kumdunga kisu mkewe kufuatia ugomvi wa kinyumbani Jumatatu usiku.

Kisa hicho ambacho kilimwacha mkewe, 25, kulazwa katika Hospitali ya Misheni ya Lwak kilifanyika katika nyumba za makazi za Kalandini KeNHA katika kaunti ndogo ya Rarieda ambazo zinakaliwa na maafisa wa CIPU.

Kulingana na kamanda wa polisi kaunti ya Siaya Cleti Kimaiyo, afisa huyo wa CIPU alizua ugomvi na mkewe na kumdunga  kisu upande wa kushoto wa tumbo kabla ya kutoweka gizani.

Kimaiyo alisema maofisa wengine wanaoishi ndani ya jengo hilo waliitikia wito wa mkewe na kumkimbiza haraka katika Hospitali ya Misheni ya Lwak ambako amelazwa kwa sasa.

Kimaiyo alifichua kuwa uchunguzi kuhusu tukio hilo umeanzishwa na DCIO wa eneo hilo ambao tayari wameshughulikia eneo la tukio na kuongeza kuwa afisa huyo anayekimbia atasakwa hivi karibuni.

Mkuu wa polisi wa kaunti hiyo alifichua kuwa mwathiriwa yuko katika hali nzuri katika hospitali ya misheni ya Lwak.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved