logo

NOW ON AIR

Listen in Live

KPLC yatangaza maeneo ambako stima zitapotea leo, Jumanne

Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Nairobi, Kericho, Busia, Nyeri, Kiambu, na Mombasa.

image
na SAMUEL MAINA

Habari09 July 2024 - 04:57

Muhtasari


  • •Kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyika kwenye mitambo.
  • •Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Nairobi, Kericho, Busia, Nyeri, Kiambu, na Mombasa.

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumanne, Julai 9. 

Katika taarifa ya Jumatatu jioni, kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyika kwenye mitambo.

Walisema baadhi ya maeneo ya kaunti tatu za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni. Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Nairobi, Kericho, Busia, Nyeri, Kiambu, na Mombasa.

Katika kaunti ya Nairobi, sehemu za mitaa ya Thigiri na Karen zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Baadhi ya sehemu za maeneo ya Chemosit na Litein katika kaunti ya Kericho zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa tisa alasiri.

Sehemu kadhaa za maeneo ya Amerikwai na Malaba katika kaunti ya Busia pia zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Maeneo ya Kaiguri Gondo, Muthinga na Karima katika kaunti ya Nyeri litashuhudia kukatizwa kwa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Katika kaunti ya Kiambu, sehemu za maeneo ya Gretsa, na mtaa wa Phase 13 zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Baadhi ya sehemu za maeneo ya Bombululu na Kisauni katika kaunti ya Mombasa pia zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved