Rais Ruto amteua Mudavadi Kuwa Kaimu Waziri Katika Wizara zote

“Kwamba kwa mujibu wa kufungu 152 (5) Katiba Wycliffe Musalia Mudavadi, ameteuliwa kuwa Kaimu waziri katika nyadhifa zote za mawaziri zilizo wazi.”

Muhtasari

•Kuteuliwa kwa Mudavadi kama Kaimu Waziri katika wizara zote zilizoachwa wazi kulitangazwa katika notisi ya serikali na Rais Ruto.

•Tangazo hilo la Rais limekuja wakati kutimuliwa kwa mwanasheria mkuu kumepingwa mahakamani, kwa hoja kwamba haikuwa ya kiutaratibu.

Rais William Ruto na Waziri Mkuu Musalia Mudavadi.
Image: Hisani

Rais William Ruto amemteua Mkuu wa Baraza la Mawaziri Musalia Mudavadi kuwa Kaimu waziri katika wizara zote zilizoachwa wazi.

Kuteuliwa kwa Mudavadi kama Kaimu Waziri katika wizara zote zilizoachwa wazi kulitangazwa katika notisi ya serikali na Rais Ruto.

“Kwamba kwa mujibu wa kufungu 152 (5) Katiba Wycliffe Musalia Mudavadi, ameteuliwa kuwa Kaimu waziri katika nyadhifa zote za mawaziri zilizo wazi.”

Jukumu jipya la Mudavadi ni muhimu katika kutekeleza maamuzi yanayohitaji mawaziri ikiwa ni pamoja na wizara ya Hazina ya Kitaifa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi ambayo yanahitaji maamuzi kadhaa kufanywa kila siku na waziri.

Tangazo hilo la Rais limekuja wakati kutimuliwa kwa mwanasheria mkuu kumepingwa mahakamani, kwa hoja kwamba haikuwa ya kiutaratibu.

Ruto aliwafuta kazi mawaziri wote na kumwachilia tu Mudavadi ambaye ni Waziri Mkuu na Waziri wa Masuala ya Kigeni.

Katika notisi hiyo, Rais pia alitangaza kufutwa kazi kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na mawaziri wote 21 wa Baraza la Mawaziri waliofukuzwa kazi Julai 11 katika kuvunjwa kwa Baraza la Mawaziri.

Rais Ruto alisema ameamua kuvunja Baraza lake la Mawaziri baada ya kutafakari, kusikiliza kwa makini kile watu wa Kenya wamesema na baada ya tathmini kamili ya utendakazi wa baraza la mawaziri na mafanikio na changamoto zake.

Rais pia alibainisha kuwa, wakati huo huo, atashiriki katika mashauriano ya kina katika sekta tofauti na miundo ya kisiasa wakati atakapounda Baraza lake la Mawaziri lijalo.