Mwanaharakati Boniface Mwangi atiwa mbaroni

Akithibitisha kukamatwa kwake, wakili wa Mwangi alifichua kwamba mwanaharakati huyo alikamatwa

Muhtasari
  • Boniface Mwangi alikamatwa pamoja na mwanaharakati mwenzake Hussein Khalid wa Haki Africa walipokuwa wakipinga mauaji ya hivi majuzi yaliyoshuhudiwa wakati wa maandamano dhidi ya serikali.
Boniface Mwangi
Boniface Mwangi
Image: HISANI

Mwanaharakati Boniface Mwangi Alhamisi aliripotiwa kukamatwa na maafisa wa polisi alipokuwa akiandamana katika Kenyatta Market jijini Nairobi.

Akithibitisha kukamatwa kwake, wakili wa Mwangi alifichua kwamba mwanaharakati huyo alikamatwa na kupelekwa katika Kituo Kikuu cha Polisi.

Boniface Mwangi alikamatwa pamoja na mwanaharakati mwenzake Hussein Khalid wa Haki Africa walipokuwa wakipinga mauaji ya hivi majuzi yaliyoshuhudiwa wakati wa maandamano dhidi ya serikali.

Huku ikitoa wito wa kuachiliwa kwao, Tume ya Haki za Kibinadamu ya Kenya (KHRC) iliapa kuendelea kupigania kukamatwa kwa maafisa hao ambao waliripotiwa kuwaangusha waandamanaji wanaoipinga serikali.

"Mwachilie  Boniface Mwangi na Hussein Khalid. Hatutaacha kutaka maafisa waliohusika na vifo vya Wakenya wasio na hatia wawajibishwe," Tume ilibaini.

Muda mfupi kabla ya kukamatwa kwake, mwanaharakati huyo anaweza kunaswa akiandamana katika Wilaya ya Kati ya Biashara ya Nairobi (CBD) pamoja na waandamanaji wengine huku akiwa ameshikilia mabango makubwa na misalaba.

Waandamanaji hao walikuwa wamevalia fulana nyeupe zilizokuwa na mistari nyekundu.