logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nairobi: Utahitaji kulipia leseni ya Sh200 kila mwaka ikiwa wewe ni mpenzi wa kufuga paka

Mpango huu unalenga kuunda njia ya kimfumo ya kufuatilia na kudhibiti idadi ya paka jijini Nairobi

image
na Davis Ojiambo

Habari25 July 2024 - 11:56

Muhtasari


    Wanasayansi wapata dawa ya upangaji uzazi kwa paka.

    Wamiliki wa paka jijini Nairobi sasa watahitajika kulipa Sh200 kama ada ya leseni kwa serikali ya kaunti.

    Kwa mujibu wa ripoti hiyo kwenye People Daily, Haya ni miongoni mwa mapendekezo yaliyomo katika Mswada wa Kudhibiti Wanyama na Ustawi wa Kaunti ya Jiji la Nairobi 2024.

    Mswada huo unaangazia vipengele mbalimbali vya utunzaji, udhibiti na ustawi wa wanyama, unaolenga kuunda hali ya kuishi pamoja kati ya wakazi na wanyama.

    Mswada huo ambao unatazamiwa kuanza kutekelezwa baada ya kuidhinishwa na Gavana Johnson Sakaja, unatazamiwa kushirikishwa na umma mnamo Agosti 2.

    Kulingana na Mswada huo, wamiliki wa paka watalazimika kuhuisha leseni hizo kila mwaka, na kuhakikisha kwamba paka wote wanasasishwa na chanjo ya kichaa cha mbwa na wanatunzwa katika hali ambayo inakuza ustawi wao.

    Mchakato wa utoaji leseni umeundwa kuwa moja kwa moja, huku wamiliki wakihitaji kutoa uthibitisho wa chanjo na kulipa ada ya kawaida.

    Mpango huu unalenga kuunda njia ya kimfumo ya kufuatilia na kudhibiti idadi ya paka jijini Nairobi, kupunguza matukio ya paka waliozurura na kutelekezwa.


    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved