logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbunge wa zamani akamatwa na dola ghushi za Marekani katika msako uliolenga mkewe kuhusu NHIF

Oparesheni hiyo ililenga washukiwa saba, akiwemo mke wa mbunge huyo,

image
na Davis Ojiambo

Habari26 July 2024 - 09:12

Muhtasari


  • •Mkewe alikuwa miongoni mwa  washukiwa wakuu  waliolaghai hazina ya kitaifa ya bima ya hospitali (NHIF) zaidi ya Ksh.199 milioni.
  • •Hata hivyo pia alikamatwa baada ya kupatikana na dola gushi za Marekani wakati wa upepelezi kwenye nyumba yao

Tume ya maadili na kupambana na ufisadi (EACC) imemkamata aliyekuwa mbunge Kutoka Kaskazini Mashariki na mkewe.

Inadaiwa  kuwa mwanasiasa huyo aliwafyatulia risasi makachero wa tume ya maadili na kupambana na ufisadi (EACC) waliokuwa wameenda nyumbani kwake katika msako uliomlenga mkewe.

Katika taarifa ya EACC, mkewe  alikuwa mshukiwa mkuu wa sakata ya mamilioni ya fedha katika shirika la a kitaifa wa bima ya afya (NHIF).

Mbunge huyo wa zamani aliwafyatulia risasi maafisa wa upelelezi wa EACC walipokuwa wakijaribu kuingia nyumbani kwake, lakini hatimaye alikamatwa pamoja na mkewe.

 

"Wanandoa hao walikamatwa Alhamisi alasiri baada ya mbunge huyo kudaiwa kuwafyatulia risasi maafisa wa upelelezi wa EACC waliokuwa wameenda nyumbani kwake kwa ajili ya msako unaomlenga mkewe, mshukiwa mkuu wa sakata ya mamilioni ya NHIF inayochunguzwa na tume," EACC ilisema.

Upekuzi katika nyumba hiyo ulifanikisha kupatikana kwa mabegi yaliyokuwa na Dola za Marekani bandia zinazokadiriwa kuwa na thamani ya mamilioni ya fedha pamoja na kemikali mbalimbali.

"Wakati wa operesheni hiyo, wapelelezi walipata mikoba miwili iliyojaa dola za Kimarekani, zinazokadiriwa kuwa mamilioni, na kemikali mbalimbali (zikiwa za unga na kioevu) zinazoshukiwa kutumika kutengeneza noti bandia. Sampuli za noti zilizojaribiwa katika taasisi ya uchunguzi ya kifedha ya EACC. Maabara zilikuwa ghushi," EACC iliongeza.

Mbunge huyo wa zamani na mkewe walikabidhiwa kwa kurugenzi ya upelelezi wa makosa ya Jinai (DCI) pamoja na vitu vilivyopatikana na bastola aina ya Ceska yenye leseni iliyoisha muda wake.

Kulingana na EACC, oparesheni hiyo ililenga washukiwa saba, akiwemo mke wa mbunge huyo, meneja wa NHIF tawi la Eastleigh na wakurugenzi watano wa duka la dawa la Beirut Pharmacy, ambao kwa njia ya ulaghai walijipatia Sh199 milioni kutoka NHIF kupitia madai ya uwongo yaliyowezeshwa na maafisa wa NHIF.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved