- “Chama cha UDA kinazingatia demokrasia na utawala wa sheria. Mheshimiwa Salah Yakub ana haki ya kushinikiza marekebisho hayo
Seneta wa kaunti ya Nandi Samson Cherargei amesema ataunga mkono pendekezo la kuondoa muhula wa kuhudumu wa rais iwapo litawasilishwa katika bunge la Seneti.
Kupitia mtandao wake wa Twitter Jumatano, Cherargei aliongeza kuwa mbunge wa Fafi Salah Yakub aliyetoa pendekezo hilo ana haki ya kushinikiza marekebisho hayo.
“Chama cha UDA kinazingatia demokrasia na utawala wa sheria. Mheshimiwa Salah Yakub ana haki ya kushinikiza marekebisho hayo, ni vyema tumsikilize kwanza, nitaunga mkono pendekezo hilo katika bunge la Seneti. Hili ni swala ambalo linaweza likajadiliwa siku za usoni,” alisema Seneta Cherargei.
Pendekezo la mbunge huyo wa chama cha UDA limeibua hisia mseto miongoni mwa wakenya na pia katika ulingo wa kisiasa.
Hata hivyo cham hicho kilikana madai hayo siku ya Jumanne, kupitia kwa mwenyekiti wao Muthama
Mbunge Yakub alisema kuwa atawasilisha mswada bungeni ili kuona kwamba kipengele hicho kinafutiliwa mbali na badala yake kubadilishwa na kipengele cha umri wa rais atakayekuwa akihudumu madarakani.
UDA is an epitome of democracy & rule of law. Hon. Salah Yakub is within his right to push this ammendment let's listen first, i shall support in the senate. This is a conversation that might happen in future by Kenyans on scrapping of term limit of a President.
— Senator Kiprotich Arap Cherargei (@scherargei) November 9, 2022
Kazi Ni kazi. pic.twitter.com/nIanQyOvB0