logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ruto anapeleka nchi katika mwelekeo ufaao-Wahome Thuku akiri

Ijapokuwa Wahome Thuku kwa sasa anaunga mkono kambi ya Azimio ya Raila Odinga

image

Habari15 September 2023 - 12:37

Muhtasari


  • Kupitia akaunti yake rasmi ya Facebook, Wahome Thuku alikiri kwamba anadhani Rais William Ruto anaipeleka nchi katika mwelekeo ufaao.

Tangu kufanyika kwa hendisheki kati ya aliyekuwa Rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga mnamo 2018, mambo hayajawahi kuwa sawa tena kati ya Uhuru na Rais William Ruto.

Viongozi hao wawili wakuu na washirika wao wamekuwa wakirushiana vijembe na maneno makali na mmoja wa washirika wa Uhuru ambaye amekuwa akimsababishia matatizo ya kila aina Ruto ni Wahome Thuku.

Ijapokuwa Wahome Thuku kwa sasa anaunga mkono kambi ya Azimio ya Raila Odinga, amekuwa akiweka wazi kuwa yuko Azimio pekee kwa sababu ya Uhuru na hivyo basi, amekuwa akielekeza bunduki yake kwa serikali ya Rais William Ruto lakini leo amewashangaza Wakenya baada ya matamshi yake ya hivi punde.

Kupitia akaunti yake rasmi ya Facebook, Wahome Thuku alikiri kwamba anadhani Rais William Ruto anaipeleka nchi katika mwelekeo ufaao.

Aliendelea kusema kuwa anajua watu wengi hawawezi kuamini kuwa anaweza kusema maneno kama hayo lakini kulingana na takwimu zake za mfumuko wa bei, Ruto yuko kwenye njia sahihi.

"HABARI ZA ASUBUHI Watu kadhaa wameniuliza swali hili, "Wahome unafikiri tunaelekea wapi?" Na nimewajibu kwa njia nyingi kama nilivyoweka kwenye Kameme FM Jumatano. Wacha niwe mkweli jinsi ninavyowajibu, nadhani William anatupeleka mahali fulani. Ndio na mimi sio mbishi. Nina hakika huwezi kuamini kuwa ni mimi nikisema hivi kwa hivyo ninatarajia maoni ya "umenunuliwa" kwa wingi, lakini takwimu ziko hapa. MFUMUKO wa bei umepungua kwa miezi kadhaa. Mwisho wa Mei 2023 ilikuwa 8.03%. Mwisho wa Juni 7.88% Mwisho wa 7.28% Mwisho wa 6.73%,"Thuku alisema.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved