logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waititu asema Ruto ana mambo 2 ya kufanya baada ya maandamano ya Gen Z

Rais wa Tunisia Zine El Abidine Ben Ali alikimbilia Saudi Arabia tarehe 14 Januari 201

image

Habari03 July 2024 - 12:43

Muhtasari


  • Kulingana naye, kuwafuta kazi washirika wake ndiyo njia pekee ambayo watu watarejesha matumaini kwake.
Aliyekuwa gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu

Aliyekuwa Gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu amemshauri rais aidha kujiuzulu au kuwafuta kazi makatibu wake wote wa baraza la mawaziri, na uongozi wa juu kuhusiana na hadhi ya taifa kwa sasa.

Kulingana naye, kuwafuta kazi washirika wake ndiyo njia pekee ambayo watu watarejesha matumaini kwake.

Waititu aliendelea na kueleza kuwa kinachoendelea si cha kipekee nchini Kenya, kilitokea Misri na Tunisia, na kusababisha kujiuzulu kwa viongozi wao.

“Kinachotokea si cha Kenya pekee, kilitokea Misri na Tunisia na kusababisha kujiuzulu kwa viongozi wao. Suluhu pekee alilonalo rais ni kujiuzulu au kuwafuta kazi makatibu wake wote wa baraza la mawaziri na uongozi ili watu warudishe matumaini kwake,” alisema.

Rais wa Tunisia Zine El Abidine Ben Ali alikimbilia Saudi Arabia tarehe 14 Januari 2011 kufuatia maandamano ya Mapinduzi ya Tunisia. Rais wa Misri Hosni Mubarak alijiuzulu tarehe 11 Februari 2011 baada ya siku 18 za maandamano makubwa, na kumaliza miaka 30 ya urais wake.

Vijana wa Kenya wamekuwa wakipanga kwenye mitandao ya kijamii maandamano ya amani mitaani yaliyokusudiwa kulazimisha mamlaka kufuta mswada wa fedha wa 2024. Maandamano hayo yalianza Juni 18 baada ya mswada huo kuwekwa hadharani kwa mara ya kwanza.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved