logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pango lililogunduliwa mwezini linaweza kuwa makao ya wanadamu

Wanasayansi kwa mara ya kwanza wamegundua pango kwenye Mwezi.

image
na SAMUEL MAINA

Habari16 July 2024 - 12:41

Muhtasari


  • •Ni moja tu kati ya mamia ya mapango yaliyofichwa katika "ulimwengu wa chini ya ardhi, ambao haujagunduliwa", kulingana na watafiti.

Wanasayansi kwa mara ya kwanza wamegundua pango kwenye Mwezi.

Pango hilo lenye kina cha mita 100, linaweza kuwa mahali pazuri kwa wanadamu kujenga makao ya kudumu, wanasema.

Ni moja tu kati ya mamia ya mapango yaliyofichwa katika "ulimwengu wa chini ya ardhi, ambao haujagunduliwa", kulingana na watafiti.

Nchi zinakimbia ili kupata makao kudumu wa binadamu mwezini, lakini zitahitaji kuwalinda wanaanga dhidi ya mionzi, halijoto kali na hali ya hewa ya anga.

Helen Sharman, mwanaanga wa kwanza wa Uingereza kusafiri angani, aliiambia BBC News kwamba pango hilo jipya lililogunduliwa lilionekana kama mahali pazuri kwa makao na alipendekeza kuwa wanadamu wanaweza kuwa wanaishi kwenye mashimo ya mwezi katika miaka 20-30.

Lakini, alisema, pango hili ni la kina sana hivi kwamba wanaanga wanaweza kuhitaji kujificha ndani na kutumia " lifti" ili kutoka.

Lorenzo Bruzzone na Leonardo Carrer katika Chuo Kikuu cha Trento nchini Italia walipata pango hilo kwa kutumia rada kupenya shimo kwenye uwanda wa mawe unaoitwa Mare Tranquillitatis.

Inaonekana kwa macho kutoka Duniani, na pia ndipo Apollo 11 ilitua mnamo 1969.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved