- Nairobi inaongoza kwa visa 227
- Idadi ya walioaga dunia leo ni 16
Watu 497 wamepatikana na virusi vya corona baada ya sampuli 4,888 kupimwa katika saa 24 zilizopita .Idadi hiyo sasa inafikisha 46,144 jumla ya visa vya ugonjwa huo nchini . Jumla ya sampuli zilizopimwa hadi sasa ni 632,669.Kutoka visa hivyo 471 ni vya wakenya huku 26 vikiwa vya raia wa kigeni .mgonjwa wa umri wa chini ni mtoto wa mwaka mmoja ilhali wa umri wa juu ana umri wa miaka 88 .
Watu 295 waliopatikana na ugonjwa huo ni wanaume ilhali 202 ni wanawake
Leo watu 238 wamepona na kufikisha jumla ya watu waliopona corona nchini kuwa 32,760 .
Hata hivyo watu 16 wameaga dunia na kufikisha idadi ya walioangamia kwa ajili ya corona kuwa 858 .
Kwa sasa kuna wagonjwa 27 katika kitengo cha wagonjwa mahtuti ilhali 27 wapo katika usaidizi wa kupumua na 41 wanasaidiwa na gesi ya kupumua .