Ulaghai wa simu

Afisa wa gereza akamatwa na kadi 10,000 za simu

Mshukiwa yupo seli akingoja kufikishwa kortini

Muhtasari
  • Askari wa jela akamatwa na kadi za simu 
  • Ulaghai wa kupitia simu na mtandao umezidi nchini 

 

Maafisa wa DCI wamemkamata afisa mmoja wa maghereza  Constable  Charles Opollo Ndaga katika mtaa wa  Sinapanga huko Bondo kwa usajili haramu wa kadi za simu

Walipokagua nyumba yake walizipata kadi 10,000 za simu ,simu kadhaa za rununu na kitabu cha  hundi . Kadi mbili za simu za  Equitel  na vitambulisho  vitatu vilipatikana pia .

 Mshukiwa yupo  katika kizuizi cha  polisi akingoja kufikishwa kortini . Katika tukio jingine kama hilo ,mshukiwa  mmoja alikamatwa siku ya jumapili huko Taita taveta kwa  ujasusi wa mtandaoni . mshukiwa huyo  Archibald Kalela Mwandawiro  mwenye umri wa miaka 52  alikamatwa Wundanyi ambapo polisi walinasa kifaa  kinachotumiwa  kunasa mawasiliano ya mtandao

 Wakati wa oparesheni hiyo  vifaa 25 vya modem  ,kadi 83 za simu za airtel ,kadi 76 za simu za  safaricom  ,tarakilishi bebe  na simu ya rununu  pamoja na vifaa n vilinaswa