BBI

Uhuru apigia debe ripoti ya BBI Kisumu

Uhuru na Raila wapigia debe ripoti ya BBI

Muhtasari
  •  Uhuru amesema wakenya wanafaa kuisoma na kuinga mkono ripoti ya BBI 
  • Amesema ripoti hiyo itawaunganisha wakenya 

 

Rais Uhuru Kenyatta amewataka wakaazi wa kisumu kuunga mkono ripoti ya BBI . Uhuru siku ya alhamisi amewataka wakaazi kuisoma  na kuielewa ripoti hiyo  na kutembea pamoja na wakenya wengine kwani ripoti hiyo itawaunganisha wakenya .

 Uhuru alikuwa akizungumza katika  uwanja wa Kisumu Showground wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa uwanja wa  Michezo wa kimataifa wa Jomo Kenyatta katika  uwanja wa Mamboleo

 amesema uwanja huo wa maonyesho utabadilishwa kuwa uwanja mkubwa wa  michezo huku viwanja vingine vya michezo nchini vikifanyiwa ukarabati .

 amesema baada ya uwanja huo kutamatika utakuwa mwenyeji wa mchuano mkali kati ya Gor Mahia na Afc Leopards aprili mwaka ujao .

" Tulikatathmini kwamba uwanja wa Jomo Kenyatta haukutosha kuwa wa kimataifa na ndiposa baada ya mashauriano na gavana  na wadau wengine  tuliamua kuubadilisha uwanja huo wa maonyesho kuwa  uwanja wa kimataifa ‘Uhuru amesema

Uhuru  amesema yeye na Raila wataongoza kampeini za kuwataka wakenya kuunga mkono ripoti ya BBI .