Jumwa yuko huru

Aisha Jumwa aachiliwa kwa dhamana ya shilingi milioni 4 pesa taslimu

Ameshtakiwa kwa mauaji

Muhtasari
  •  Jumwa ameshtakiwa kwa mauaji 
  •  Ametakiwa kusalimisha paspoti yake kortini 

 

Mbunge wa Malindi Aisha Jumwa

Mbunge wa Malindi Aisha Jumwa  ameachiliwa kwa bondi ya shilingi milioni 3 au dhamana ya shilingi milioni nne pesa taslimu

Mlinzi wake  Geoffrey Otieno  aliachiliwa kwa bondi ya shilingi milioni moja au dhamana mdadala ya shilingi milioni 1.5 pesa taslimu .

Jaji Njoki Mwangi amewaagiza washtakiwa kuwasilisha paspoti zao kortini . Amesema wataruhusiwa tu kusafiri endapo watatoa sababu tosha za kuruhusiwa kusafiri .

Mwangi pia amewaonya dhidi ya kuwatishia mashahidi  wa upande wa mashtaka .Jumwa  na msaidizi wake watatakiwa kufika kortini kila wakati mahakama itakapowataka kufanya hivo .

Jumwa  ameshtakiwa pamoja na Otieno ka kumuua Gumbao Jola  mwanamme mwenye umri wa miaka 48  katika kijiji cha Ganda Oktoba mwaka wa 2019 . Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma wa Mombasa  Alloys Kemo alipinga kuachiliwa kwa wawili hao wa dhamana .

Kemo  amesema Jumwa ni mtu mwenye ushawishi mkubwa na atavuruga  mashahidi wa upande wa mashtaka  ambao wanategemewa katika kesi hiyo dhidi yake .Pia alisema Otieno hana makaazi ya kudumu na hivyo basi itakuwa ni hatari kwa mahakama kumuachilia huru .