Uhuru akutana na BAK

Uhuru awaonya wahudumu wa boda boda dhidi ya kutumiwa vibaya na wanasiasa wakati wa kampeni

Amesema wanasiasa wasiwatumie boda boda vibaya

Muhtasari

 

  • Rais amesema serikaliz itazidi kuwaunga mkono wahudumu wa boda boda 

 

 

Rais Uhuru Kenyatta amewashauri wahudumu wa boda boda dhidi ya kutumiwa vibaya na wanasiasa kuafiia malengo yao  ya kibinafsi .

Uhuru  ameitaja sekta ya boda  kama yenye uwezo mkubwa  iwapo mikakati itawekwa kutumia vyema michango ya  kila siku ya fedha zao .

 Amewapa  amewarai wahudumu hao  kusalia macho ili wasitumiwe vibaya  na wanasiasa ambao wanawapa  pesa ambazo haziwezi kuwasaidia .

 Rais aliyasema hayo siku ya ijumaa  wakati alipokutana na muungano wa usalama wa wana boda boda  katika  Ukumbi wa kijamii wa Pumwani .

 Aliongoza kusainiwa kwa mkataba  muhimu kati ya  Muungano huo BAK , Maamlaka ya mtaji nchini ,Rubis Energy  na Nabo Capital .

 Amewashauri wahudumu wa boda boda kuwekeza  vizuri kutumia kiasi kikubwa cha fedha ambazo wao hupata kila siku  lakini kwa kinaya bado wengi wao ni maskini .

 Rais alisema sekta ya boda boda ni muhimu sana kwani takriban watu milioni 22 hutumiwa usafiri wa boda boda kila siku .

Uhuru  amesema sekta hiyo hupata  kiasi cha  shilingi bilioni  357 kila mwaka  ,kiasi ambacho kinazidi hata mgao unaopewa serikali za kaunti