Muhtasari
- Naironi ina visa 556
- 14 wafariki
Kenya siku ya jumanne imesajili visa vipya 836 vya corona huku watu 14 zaidi wakiaga dunia kwa ajili ya ugonjwa huo na kufikisha idadi ya walioangamizwa na virusi hivyo kuwa 934 . Idadi ya walioambukizwa sasa imesonga watu 50,833. Watu 618 ni wanaume ilhali wanawake ni 218 .Mgonjwa wa umri wa chini ni mtoto wa miezi minn ilhali wa umri wa juu ana miaka 89
Idadi hiyo ni kutoka sampuli 4,076 zilizopimwa katika saa 24 zilizopita
Habari njema leo ni kwamba watu 403 wamepona na kufikisha jumla ya idadi ya walipona corona hadi sasa kuwa 34,832
Kwa sasa watu 1,150 wamelazwa katika hospitali mbali mbali ilhali 3,961 wapo katika utunzi wa nyumbani.Wagonjwa 38 wapo ICU ilhali 25 wapo katika kitengo cha HDU .