- Muigai Amelionya baraza hilo la wazee dhidi ya kuunga mkono mrengo wowote wa kisiasa
- Mapema mwezi Oktoba Muigai aliyataka makundi ya wazee wa kijamii kuhakikisha kwamba kuna umoja wa kitaifa .
Naibu wa rais William Ruto amekutana na viongozi wa baraza la kitaifa la wazee wakiongozwa na mkuu wa baraza hilo Kung’u Muigai .
Miongoni mwa waliojiunga na wazee hao ni mwenyekiti Phares Rutere
Muigai ni binamu yake rais Uhuru Kenyatta .Maajuzi Migai amewashtumu wazee wa jamii ya Kikuyu ambao walisafiri hadi Bondo kwa mkutano katika boma la kiongozi wa ODM Raila Odinga . Amelionya baraza hilo la wazee dhidi ya kuunga mkono mrengo wowote wa kisiasa
Mapema mwezi Oktoba Muigai aliyataka makundi ya wazee wa kijamii kuhakikisha kwamba kuna umoja wa kitaifa .
“ Kama wazee hatufai kujiingiza katika siasa ndogo ndogo .Msimamo wetu ni kwamba Viongozi wote wa kisiasa ni watoto wetu na ukiwapata watoto wako wakipigana,je utachukua kiboko na kuanza kumchapa mmoja wao?’ alihoji .
Wakati wa mkutano wa Karen na Ruto ,naibu wa rais alisema kwamba wazee wanafaa kuwa mstari wa mbele kuleta umoja na kumaliza ukabila nchini .
Ruto amesema wazee wakihusika na mchakato mzima wa kuleta utangamano basi Kenya itaafikia maendeleo yafaayo na kuwa na Amani