Corona bungeni

Bunge la kaunti ya Mombasa lasitisha vikao baada ya wawakilishi watatu kupatikana na corona

Likizo hiyo sasa itadumu siku 14 zaidi

Muhtasari
  •  Wakilishi watatu wapatikana na corona 
  • Bunge lilifaa kurejelea vikao vyake jumatatu 
  • waakilishi wa kaunti  walioambukziwa kujitenga 

 

 Taharuki imetanda katika bunge la kaunti ya Mombasa baada ya wakilishi watatu wa wadi kupatikana na virusi vya corona .  Likizo ya wiki mbili ya viongozi hao sasa imongezwa kwa siku 14 zaidi .wakilishi  hao walifaa kurejea kazini siku ya jumatatu  .Naibu spika Fadhili Makarani  alithibitisha   maambukizi hayo na kusema kwamba siku hizo 14 zinaweza kuzidishwa kuwa 21 .

 “ Tuna wakilishi watatu wa wadi ambao wameptikana na virusi vya corona  ndio kwa sbaabu tumeamua kuzidisha muda wa likizo kwa wiki mbili  ili wajiteng’ amesema Makarani .

 Wakilishi wa kaunti  sasa wapo hatarini kwani walifichwa kuhusu  maambukizi hayo kwa sababu zoezi la kuwapima lilikomeshwa kwa ajili ya gharama yake ya ‘juu’

 Makarani hata hivyo  amesema kuna wafanyikazi ambao wapo kazini na watahitaji kupimwa .

 Amesem,a kwa sababu ya unyanyapaa unaomatana na watu kupatikana na ugonjwa huo waliamua kutotoa maelezo hayo kwa njia ambayo ingzua hofu miongoni mwa wafanyikazi wa kaunti . Amesema uongozi wa bunge la kaunti hiyo utachukua hatua za kuhakikisha kwamba kila mtu anapimwa .