Afueni

Sudan yapata afueni baada ya Amerika kuondolea vikwazo vya miaka 23

mwisho wa vikwazo kwa Sudan

Muhtasari

 

 Sudan sasa kufanya biashara na kampuni za Amerika 

 

waziri mkuu wa Sudan Abdullah Hamdok na katibu wa mashauri ya kigeni wa Marekani Mike Pompeo

 

Serikali ya  Marekani siku ya jumatatu imeondolea Sudan vikwazo  vya muda wa miaka 23  baada ya nchi hiyo kupa akutounga mkono  vitendo vya kigaidi  siku zijazo .

 Rais Donald Trump  kupitia taarifa amesema  hatua hiyo imechukuliwa baada ya Sudan kukubali  kutoa fidia ya Dola milioni 335 kwa waathiriwa wa mashambulizi ya kigaidi . Vikwazo hivyo vimeizuia Sudan kufanya biashara yoyote kutumia sarafu ya dola au kununua bidhaa za kutoka Marekani .

 Hatua hiyo ilimaanisha kwamba hakuna kampuni za Amerika zilizotaka kufanya biashara na Sudan kwa kipindi hicho hali ambayo ilichangia kuzorotesha uchumi wa nchi hiyo  huku  mashirika ya serikali kama vile ye ndege na viwanda vikikosa kununua vifaa na kupewa huduma za ukaraat na biashara za Marekani na washirika wake .

 Baada ya kuafikiwa makubaliano hayo ,Sudan sasa ipo huru kufanya mikataba na kampuni za Marekani na mataifa  mengine ya magharibi  kwa mara ya kwanza tangia mwaka wa 1997 wakati vikwazo hivyo vilipotangazwa