Afueni

Korti ya rufaa yafutilia mbali uamuzi wa mahakama kuu kufuta uchaguzi wa mbunge Anne Wanjiku

Muhtasari
  • Mahakama kuu ilikuwa imesema hakuchaguliwa kwa njia ifaayo
  •  Sasa uamuzi wa jaji Korir umesimamishwa hadi rufaa iamuliwe 

 

 

Mbunge Anne Wanjiku

 Mahakama ya rufaa imefutilia mbali uamuzi wa mahakama kuu uliokuwa umetupilia mbali uchaguzi wa mbunge wa gatundu Kaskazini Anne Wanjiku .

Wanjiku  kupitia wakili wake Tom Ojienda  alikuwa amewasilisha rufaa  akisema hakuridhishwa na  uamuzi uliotolewa na jaji Weldon Korir ambaye alikitangaza kiti chake kuwa wazi .

 

 Mnamo oktob tarehe 7  Jaji Korir  alisema kwamba Wanjiku hakuwa  amechaguliwa kwa njia ifaayo kwani wakati huo alikuwa yungali akihudumu kama mwakilishi wa kaunti .

 Majaji Martha Koome , Daniel Musinga na Sankale Ole Kantai wamesimamisha uamuzi wa Korir hadi  uamuzi wa rufaa hiyo utolewe .