- Oparanya achukua hatua baada ya visa kuongezeka
- Serikali kuu pia inahofishwa na ongezeko la idadi ya waliombukizwa
Makao makuu ya kaunti ya kakamega yamefungwa kwa wiki moja kufuatia ongezeko la visa vya corona katika siku za hivi karibuni .
Gavana Wycliffe Oparanya ametangaza siku ya jumatano kusitishwa kwa shughuli zote katika afisi za makao makuu ya kaunti na kuagiza kwamba wafanyikazi wote wapimwe ugonjwa huo .
Hatua hiyo inajiri siku moja tu baada ya bunge la kaunti hiyo kusitisha shughuli zake kwa wiki mbili baada ya wakilishi watatu wa wadi kupatikana na virusi vya corona .
Kaunti hiyo ina jumla ya visa 316 vya corona huku 57 vikiwa vya wahudumu wa afya . idadi hiyo ndio ya juu Zaidi tangu kisa cha kwanza kuripotiwa nchini mwezi machi .
Miongoni mwa walioathiriwa ni maafisa wakuu katika ofisi ya oparanya .Gavana huyo amesema watu saba wameaga dunia katika kaunti ya kakamega kwa ajili ya virusi hivyo .
Oparanya amesema utunzi wa nyumbani sasa utaboreshwa kwa wote walio na virusi hivyo ili kuepuka mrundiko wa watu katika vituo vya afya . Hospitali nyingi za kakamega zimezidiwa na idadi ya juu ya wagonjwa huku visa zaidi vikiripotiwa kila siku . Wiki ijayo rais Uhuru kenyatta ataanda mkutano na magavana ili kujadili hatua Zaidi za kuchukuliwa kukabiliana na ongezeko la maambukizi ya ugonjwa huo nchini .