Kassait kwenye kiti moto

Mazimwi ya IEBC yamsakama Immaculate Kassait akihojiwa kuwa Kamishna wa Data

alikuwa akifanya kazi IEBC

Muhtasari

 

  •  Hatma yake sasa ipo mikononi mwa bunge 
  •  Rais alimteu wiki jana kuhudumu kama kamishna wa Data 
Immaculate Kassait

Maamuzi aliofanya   Immaculate Kassait wakati wa uchaguzi uliokuwa na ushindani mkali wa mwaka wa 2017 yamerejea kumsakama  wakati akihojiwa kuwa kamishna wa data alipofika mbele ya wabunge  siku ya jumatano

Kassait  ambaye amekuwa mkurugenzi wa IEBC   wa elimu kwa wapiga kura  kabla ya kuteuliwa na rais Kenyatta kuwa  kamishna wa Data  amejipata na kibarua kikubwa cha kueleza mbona anafaa kupewa kazi hiyo  kwa ajili ya mzigo wa  maamuzi ambayo yalitiliwa shaka wakati  wa uchaguzi mkuu wa 2017  ambapo  tume hiyo ilikataa kutii uamuzi wa mahakama ya juu Zaidi kufungua sava  zake ili kubaini mshindi halisi wa uchaguzi wa urais .

 Mbunge wa Mathare Anthony Oluoch  alimpa kibarua Kassait kueleza jinsi atakavyorejesha Imani ya wakenya kwake kufuatia matuko ya 2017 . Oluoch amesema  wakenya wengi hawana Imani na IEBC ,taasisi ambayo Kassait alikuwa miongoni mwa viongozi wake .

 Kassait kwa upande wake alisema atahakikisha kwamba  data ya wakenya inahifadhiwa kwa njia salama  na kulindwa  ili kutotumiwa vibaya na yeyote .

Afisi ya kamishna wa data  ina jukumu kubwa la kuhifadhi sajili na maelezo  ya wakenya pamoja na kuchunguza visa  vya utumizi mbaya wa data .

Kassait aliteuliwa kuhudumu katika nafasi hiyo na rais Uhuru Kenyatta wiki jana  na uteuzi wake utaidhinishwa iwapo wabunge watakubaliana na rais . Spika Justin Muturi  aliipa kamati ya bunge kuhusu mawasiliano jukumu la kumhoji Kassait  kabla ya kuwasilisha ripoti yake bungeni