Kakamega ,Kwale na Makueni zaongoa katika utendaji kazi

Utafiti:Kakamega ,Kwale na Makueni zaongoza katika utendakazi wa kaunti

Tana River ,Isiolo na Wajir zashika mkia

Muhtasari
  •  Utafiti watambua kaunti zenye utendaji kazi bora 
  • Kisumu , Uasin Gishu na Elgeyo Marakwet zipo katika tano bora 

 

Kaunti bora kwa utendakazi
Image: Infotrak

 

 Kaunti za  Kakamega ,Kwale na Makueni zinaongoza ktika utendakazi  kwa mujibu wa utafiti wa kura ya maoni ilioyofanywa na kampuni ya infotrak . Asilimia 57.2,54.8 na 54.4 ya wakaazi wa kaunti hizo mtawalia walionyesha kuridhika na utendakazi na utoaji huduma wa kaunti hizo tatu 

Kaunti nyingine zenye utendakazi wa juu kwa mujibu wa wakaazi wake ni  Kisumu kwa asilimia 53.4,Uasin Gishu kwa asilimia 53.1 ,West Pokot kwa asilimia 52.7 na Elgeyo Marakwet kwa asilimia 51.2

 

 Kaunti zinazoshika mkia kwa utendakazi ni  Tana River kwa asilimia 39.5,Wajir kwa asilimia 41.3,Isiolo kwa asilimia 42,samburu kwa asilimia 42.2,mandera kwa asilimia 43.1 na  Trans Nzoia kwa asilimia 43.4

 Katika utafiti huo uliohusiha jumla ya watu 37,600 kote nchini  Nyeri ndio kaunti yenye utendakazi bora  katika kaunti za  Eneo la kati kisha  Kiambu ni ya mwisho . Kwale inaongoza kwa kaunti za   pwani  nayo Tana River ni ya mwisho . Makueni inaongoza kwa kaunti za eneo la Mashariki huku  Isiolo ikishika mkia . Garissa inaongoza kwa kaunti za kaskazini mashariki ,Kisumu inaongoza kwa kaunti za Nyanza ,Uasin Gishu inaongoza kwa kaunti za Rift valley  Ilhali Kakamega ndio inayoongoza kwa kaunti za Magharibi huku Busia ikishika mkia kwa utendakazi