Afueni kwa Weta

Wetangula apata afueni baada ya kundi pinzani kuahirisha mkutano mkuu

Chama hicho kimekuwa katika mzozo wa uongozi

Muhtasari
  •  Kundi la Wamunyinyi linalenga kutwaa uongozi wa FORD KENYA 
  •  Wetangula ataslia kuwa kinara hadi kundi hilo lifanye mkutano kuidhinisha mageuzi 

 

Moses Wetangula

Seneta wa Bungoma Moses Wetangula sasa anaweza kujipa pumzi baada ya  kundi hasimu linalotaka kumuondoa kama kiongozi wa chama cha Ford Kenya kuahirisha mkutano muhimu .

 Kundi hilo linaloongozwa na mbunge wa Kanduyi Wafula Wamunyini limeahiriha mkutano  wa wajumbe wa kitaifa uliofaa kuandaliwa  jumamosi  likitaka kuwepo agizo la mahakama .

 Hatua hiyo inamaanisha kwamba Wetangula ataendelea kuhudumu kama kinara wa chama hicho  hadi wakati wapinzani wake watakapoandaa mkutano wa kuidhinisha maazimio ya kumng’atua .

 Mkutano huo pia ulitarajiwa kuidhinisha mageuzi katika uongozi ambayo yalikuwa yametekelezwa mwezi mei  .Uchaguzi huo ungekuwa wa kwanza wa Ford Kenya kwa miaka tisa.

 Barza kuu la chama hicho  liliamua kumtoa Wetangula kutoka nafasi hiyo na kumpa wadhifa huo Wamunyinyi  kwa muda kabla ya kuidhinishwa na baraza la wajumbe wa kitaifa . hata hivyo katibu mkuu wa Ford Kenya na mbunge wa  Tongaren Eseli Simiyu ambaye yupo katika kambi ya Wamunyinyi amefutilia mbali mkutano huo .