Korir afunguka kuhusu kuugua Corona

Mbunge wa Lang'ata Nixon Korir afunguka kuhusu alivyopambana Corona

Aliambukizwa virusi hivyo wiki tatu zilizopita

Muhtasari

 

  •  Mbunge huyo amesema kwa sasa hali yake ni  nzuri 
  •  Korir anasema alitibiwa na kushauriwa kwenda nyumbani 

 

Mbunge wa Lang'ata Nixon Korir

 Mbunge wa Langata  Nixon Korir amefunguka kuhusu jinsi  anavyopambana na ugonjwa huo baada ya kuambukiwa wiki tatu zilizopita .Korir amefichua hali yake baada ya ripoti kuibuka kwamba amelazwa hospitalini akiugua virusi hivyo .

 “ Nilipatikana na Corona wiki tatu zilziopita .lakini nimekuwa nikijitenga katika karantini  nitakuwa nikipimwa tena kesho’ Korir ameliamvia gazeti la The Star .

 Mbunge huyo chipukizi amesema pindi alipopatikana na virusi hivyo alikwenda hospitalini na kutibia kisha akarejea nyumbani kupata nafuu .

 Amesema alipata daalili za ugonjwa huo  katika siku za mwanzo mwanzo  na akahudumiwa haraka na madaktari .

 “ Nilipata baadhi ya daalili Novemba tarehe 1,2 na 3 kiwango hangu cha pumzi kilipungua  lakini nikamudu kupata nafuu ,nilirejea nyumbani .

 Amepuuza ripoti katika mitandao ya kijamii kwamna yungali hospitalini  akiwa katika hali mahtuti .Amesema uvumi huo unaenezwa na wanablogi .