Ghasia za Uchaguzi

Kesi 72 za mauaji zimesajiliwa tangu ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007/2008 asema Kinoti

Kinoti amesema hapatatokea tena ghasia za uchaguzi

Muhtasari

 

  •  Jumatatu Kinoti alikutana na waathiriwa wa ghasia za uchaguzi 
  • Amesema idara ya DCI itawachukulia hatua wote waliotekeleza ghasia na uhalifu wakati wa uchaguzi  wa 2007/2008
Mkurugenzi mkuu wa Idara ya DCI George Kinoti

 Jumla ya kesi 72 za mauaji ,44 za kuhamishwa kutoka ardhi  na vitisho 118 zinazohusiana na ghasia za baada ya uchaguzi  tangu machafuko ya mwaka wa 2007/2008 amesema mkuu wa DCI George  Kinoti

  Kinoti ameahidi kwamba idara yake  itafuatilia yote ambayo  waathiriwa wa ghasia za baada ya uchaguzi wwalimueleza baada ya kukutana nao siku ya jumatatu katika makao makuu ya DCI .

" Tunajua walionyakua mashamba yenu na mali yenu ambao sasa wametulia  .  Tunawajua  walioua na ambao wanapita  katika makaburi  ya waliowaua ‘ amesema  Kinoti .

Kinoti  amesema  serikali imeiagiza ofisi yake kuhakikisha kwamba hakuna ghasia au maafa yanatokea

" Hebu wajaribu tena . Tutafuata ukweli  na kutayarisha faili za kuonyesha kwamba huyu ndiye aliyemuua mtu huyu’ amesema

" Hivi karibuni tutayaona matokeo ya hafla hii .Tutawatafuta .najua wanangoja uchaguzi mwingine ili kushuhudia  ghasia’