- wanafunzi 44 walikamatwa katika Nyumba ya Kithinji wakilewa siku ya jumamosi
- Washukiwa wote watasalia rumande kwa siku saba ili polisi wakamilishe uchunguzi wao
Mwenyeji wa karamuy ambako vijana 44 wadogo walikamatwa wakinywa pombe katika mtaa wa mountain view na watu wengine wawili watasalia rumande kwa siku saba ili uchunguzi ukamilishwe .
Hii ni baada ya idara ya DCI kuitisha muda Zaidi ili kufanya uchunguzi kuhusu tukio hilo lililopeleka wanafunzi 44 na mmiliki wa nyumba hiyo Milicent Kithinji kukamaywa siku ya jumamosi .
Wakati wa oparesheni hio makachero walipata pombe na bangi katika nyumba hiyo . wanafunzi hao wa shule za msingi na upili wakuwa 26 wavulana na wasichna 18 wote kati ya umri wa miaka 14 na 17
Kithinji, mwenye umri wa miaka 41 alikamatwa na polisi ili kuhojiwa kuhusu karamu hiyo . uchunguzi wa mwanzo umeonyesha kwamba watoto hao walitoka sehemu mbali mbali ikiwemo Machakos ,Kiambu na Narobi .
Kithinji na washukiwa wengine wawili walifikishwa katika mahakama ya Milimani wakati polisi walipotaka kupewa muda wa siku saba Zaidi ili wakamilishwe uchunguzi wao
Hata hivyo wakili wao Kennedy cheruiyot alisema kwamba muda huo ni mrefu sana kwani Kithinji ana tatizo la kiafya . Hakimu aliwaruhusu polisi kuwazuiliwa washukiwa wote kwa siaku saba .
Jaji pia amewaagiza polisi kumrejesha Kithinji katika nyumba hiyo ili azichukue dawa zake