Haki

Waathiriwa wa ghasia za uchaguzi kuandikisha taarifa na DCI kuanzia leo

Wakili wa waathiriwa ICC alisema wao ndio waliopata hasara zaidi

Muhtasari
  • Uchunguzi wa mwanzo umebaini kuwepo vitisho na madhila dhidi ya waathiriwa hayo ambayo mkuu wa DCI  George Kinoti atayazungumzia katika kikao na wanahabari saa nane  alasiri siku ya jumatatu .
  • Watu 1,300   walifariki wakati wa machafuko ya baada ya uchaguzi kati ya wafuasi wa rais mstaafu Mwai Kibaki na kiongozi  wa ODM Raila Odinga mwaka wa 2007

Waathiriwa wa machafuko ya zamani ya uchaguzi  leo wataanza kurekodi taarifa zao katika makao makuu ya DCI .

 Hii ni baada ya kuongezeka kwa hou ya ghasia kutoka kwa waathiriwa wa zamani wa machafuko ya baada ya uchaguzi . Uchunguzi wa mwanzo umebaini kuwepo vitisho na madhila dhidi ya waathiriwa hayo ambayo mkuu wa DCI  George Kinoti atayazungumzia katika kikao na wanahabari saa nane  alasiri siku ya jumatatu .

 Watu 1,300   walifariki wakati wa machafuko ya baada ya uchaguzi kati ya wafuasi wa rais mstaafu Mwai Kibaki na kiongozi  wa ODM Raila Odinga mwaka wa 2007

  Wakili wa waathiriwa wa ghasia hizo katika mahakama ya ICC  Fergal Gaynor,   alisema watu aliopoteza mengi Zaidi katika mahaguko hayo nchii ni waathiriwa kwani kando na kupoteza maisha ya wapendwa wao,pia walipoteza mali yao .

 Kufuatia ghasia za uchaguzi wa mwaka wa 2007/2008  naibu wa rais William Ruto alishtakiwa pamoja na mwanahabari Joshua Sang na aliyekuwa Mwenyekiti  wa ODM Henry Kosgey 

 Mashtaka kama hayo pia yaliwakabili rais Uhuru Kenyatta ,aliyekuwa mkuu wa utumishi wa umma Francis Muthaura na aliyekuwa kamishna wa polisi Hussein Ali .